• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

WASIRA AONYA WANAOTOLEA MACHO UMEYA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 26, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
WASIRA AONYA WANAOTOLEA MACHO UMEYA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira

0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na SULEIMAN JONGO,

Mkinga

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amewaonya baadhi ya wagombea udiwani walioanza harakati za kusaka uenyekiti wa halmashauri na umeya, kabla ya uchaguzi.

Amesema wanachotakiwa kufanya wanachama wa CCM wote kwa sasa ni kuhakikisha wanasaka kura za kishindo kwa Chama hususan za mgombea urais, Dk. Samia Suluhu Hassan.

Wasira alisema hayo alipozungumza na viongozi na wanachama wa CCM katika kikao cha ndani kilichofanyika wilayani Mkinga Mkoa wa Tanga.

Kikao hicho ni mfululizo wa vikao anavyoviendesha kwa kukutana na viongozi na wana-CCM kumwombea kura Dk. Samia, wagombea ubunge na udiwani waliosimamishwa na Chama kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu.

“Kwa madiwani ninawaomba sana siyo hapa Mkinga, hapa sijaambiwa huko nilikotoka madiwani wameanza kutafuta mwenyekiti wa halmashauri na huku wao wenyewe hawajachaguliwa, sasa wewe utajuaje kama utachaguliwa wewe uanze kutafuta mwenyekiti wa halmashauri.

“Acheni mambo ya kutafuta mwenyekiti wa halmashauri kwanza tuchaguane halafu mambo ya mwenyekiti wa halmashauri yatakuja baadaye,” aliagiza.

Alisema hata nafasi ya umeya hutazamwa kupitia vikao vya juu na kwamba, katika mchakato wake iwapo atabainika diwani alianza mapema Chama hakitasita kumwengua katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi hiyo.

“Wameanza, ninawaambia hapana, hata umeya tunatazama katika kamati, nitasema nilikwenda Mkinga (ni mfano) nikawaambia hawakunisikiliza na huyu ndiye alikuwa anaongoza kampeni, tunamfuta tunaweka yule ambaye alikuwa ametulia.

“Siwatishi nawaambia maneno ya kweli na maneno ya kweli nayo yana ncha kali yanaweza kuonekana kama kitisho,” alisema.

Wasira alisema uchaguzi umewadia hivyo kila mwana CCM apambane kukitafutia Chama ushindi kiendelee kushikilia dola kwa manufaa ya Watanzania.

Alisema ana imani na wananchi wa Mkinga na Tanga kwa ujumla, hivyo hana shaka watampigia kura nyingi Dk. Samia kwa kuwa amewafanyia mambo makubwa huku Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2025-2030 ikiwa imesheheni mengine mengi mazuri ambayo yatatekelezwa kwa miaka mitano ijayo

“Sasa uchaguzi upo tayari na mimi nina imani na watu wa Mkinga maana mmekuja hapa kwa wingi ni ushahidi kwamba CCM ina watu wake tena wengi.

“Nasimama hapa kwa niaba ya Dk. Samia Suluhu Hassan kuwaomba wananchi wa Mkinga na Mkoa wa Tanga kwa ujumla kumuunga mkono na kumpigia kura za kishindo,” alisema.

Wasira anahitimisha ziara yake mkoani humo leo, ambapo anakwenda mkoani Kilimanjaro kumnadi mgombea urais Dk. Samia.

Previous Post

DK. SAMIA AMEONESHA UMAHIRI KATIKA UONGOZI – DK. NCHIMBI

Next Post

DK. SAMIA ASEMA UMEME WA KUTOSHA UMEPELEKWA VIJIJINI

Next Post
DK. SAMIA ASEMA UMEME WA KUTOSHA UMEPELEKWA VIJIJINI

DK. SAMIA ASEMA UMEME WA KUTOSHA UMEPELEKWA VIJIJINI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MGOMBEA Mwenza wa Urais, Dk. Emmanuel Nchimbi, akiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Butiama, mkoani Mara. (Picha na Abdurahman Jumanne)

BALOZI DK. NCHIMBI AZURU KABURI LA HAYATI MWALIMU NYERERE

2 months ago
SERIKALI YAIPA TANO YANGA

SERIKALI YAIPA TANO YANGA

4 weeks ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.