• ePaper
Wednesday, March 18, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

STEVEN WASIRA: TAIFA HILI HALIJAWAHI KUGAWANYIKA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 16, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
STEVEN WASIRA: TAIFA HILI HALIJAWAHI KUGAWANYIKA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ELIZABETH JOHN

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira, amesema taifa halijawahi kugawanyika kama inavyodaiwa na baadhi ya watu, bali ni mitazamo tofauti inayojitokeza kutokana na uhuru wa mawazo na demokrasia iliyoimarika.

Akizungumza katika kipindi cha Morning Trumpet kinachorushwa kituo cha televisheni cha UTV, Wasira alisema madai ya kuwepo kwa mgawanyiko ni hoja zinazotokana na mitandao ya kijamii, ambazo mara nyingi hujenga taswira isiyo halisi ya hali ya kisiasa na kijamii nchini.

“Wapo wanaoeneza mitazamo kwamba, taifa limegawanyika, ukweli ni kuwa, Watanzania wameendelea kuwa wamoja. Wanaunganishwa na amani, upendo na malengo ya pamoja ya maendeleo,” alisema.

Alisisitiza kuwa, idadi kubwa ya watu wanaohudhuria mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali nchini ni ushahidi tosha kwamba, Watanzania wanaendelea kuwa wamoja.

Alisema hata wale walio nje ya viwanja, wamekuwa wengi kuliko waliopo ndani, jambo linaloonesha hamasa kubwa ya wananchi kushiriki masuala ya kitaifa.

Aliongeza kuwa, ni haki ya msingi kwa wananchi, kuwa na maoni tofauti kuhusu masuala ya kisiasa au maendeleo, tofauti hizo, haziwezi kuwa, kigezo cha kudhani taifa limegawanyika, kwani kila nchi yenye demokrasia, haiwezi kukosa sauti tofauti.

Wasira, alisema serikali imeendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi zake kwa wananchi, ukiwemo uboreshaji wa huduma za kijamii kama elimu, afya, nishati na miundombinu, jambo linaloonesha dhamira ya dhati ya kuhakikisha ustawi wa Watanzania wote.

“Tumefanya mengi, hasa sekta za nishati na elimu. Tuliahidi kumaliza changamoto ya umeme na sasa, Bwawa la Umeme linaendelea kujengwa, jambo litakaloongeza upatikanaji wa nishati nchini,” alisema.

Pia, alisema dhamira ya serikali ni kujenga uchumi jumuishi, unaowagusa Watanzania wote, bila kujali makundi yao, wakiwemo wakulima, wafugaji, wavuvi, machinga na wajasiriamali wadogo, kuongeza kipato na ajira nchini.

Vilevile, aligusia ajenda ya katiba mpya, akisema bado ipo mezani, itajadiliwa kwa umakini zaidi baada ya uchaguzi, kwa kushirikisha vyama vya siasa na wadau mbalimbali, kuhakikisha matokeo yake yanakubaliwa na wote.

Alisema licha ya changamoto zilizopo, serikali imeendelea kushughulikia masuala ya usalama, maoni ya wananchi na marekebisho ya sheria, kuhakikisha kila Mtanzania, ananufaika na maendeleo ya taifa.

“Matatizo yapo, hakuna nchi isiyo na changamoto, tumeamua kuyashughulikia kwa umakini. Muhimu ni umoja na nia njema ya kujenga taifa letu,” alisema.

Aliwataka wananchi, kuendelea kudumisha amani, mshikamano na kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu, akisema mamlaka yote ya kuongoza nchi, iko mikononi mwa wananchi kama inavyosema Ibara ya nane ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Previous Post

DK. MWINYI AAHIDI KITUO CHA HUDUMA WENYE ULEMAVU

Next Post

DK. SAMIA AWAPA KICHEKO KARAGWE

Next Post
DK. SAMIA AWAPA KICHEKO KARAGWE

DK. SAMIA AWAPA KICHEKO KARAGWE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SEKTA YA UCHUKUZI YAPAA

SEKTA YA UCHUKUZI YAPAA

3 weeks ago
JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

JESCA MAGUFULI AWATAKA SHINYANGA KUIAMINI CCM

6 months ago

Popular News

  • MANDONGA AJA KIVINGINE

    MANDONGA AJA KIVINGINE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU AWAWEKA MTEGONI VIGOGO WILAYA, HALMASHAURI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALAMA TATU KUMUENZI JPM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUIFANYA TANZANIA KITOVU CHA BIASHARA – DK. YONAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?