• ePaper
Monday, June 8, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

ICHAGUENI CCM  – DK. MWINYI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
October 25, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
ICHAGUENI CCM  – DK. MWINYI

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,

Zanzibar

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewaomba wananchi kuhakikisha kuwa, wanajitokeza kwa wingi Oktoba 29, mwaka huu kuipigia kura CCM.

Dk. Mwinyi, aliyasema hayo katika mkutano wa kufunga kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa upande wa Zanzibar, Viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Unguja.

Alisema kampeni ni jambo moja na kupiga kura ni hatua muhimu ambayo itakihakikishia Chama ushindi wa kishindo.

Pia, alisema kampeni zimefanywa kwa ustaarabu mkubwa na kwamba, wameyafikia makundi yote, kila walipopita wananchi waliahidi kukipatia Chama ushindi.

Aidha, Dk. Mwinyi, alitumia nafasi hiyo, kujiombea kura na kumwombea kura Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia na wagombea wa ubunge, uwakilishi na udiwani wa CCM.

DK. SHEIN

Rais wa Zanzibar mstaafu na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Dk. Ali Mohammed Shein, alisema uchaguzi ni tukio la hesabu na zinazohesabiwa ni kura zinazopigwa na mwenye kura nyingi ndiyo mshindi.

Alisema kwa vuguvugu aliloliona katika kampeni za CCM bara na Zanzibar, wingi wa wanaCCM na wananchi waliohudhiria katika mikutano hiyo, inadhihirisha kuwa, ushindi wa kishindo hauna shaka.

Pia, alisema ni lazima wananchi wakapige kura kwa kuzingatia amani, utulivu umoja na mshikamano na kuwataka wakishapiga kura kila mmoja atulie nyumbani kwake akisubiri matokeo.

Aliongeza kuwa, wananchi wakapige kura kwa lengo kuimarisha Muungano kwani ndiyo hazina ya nchi na jukumu kubwa la maendeleo.

Naye, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mjini, Talib Ali Talib, alisema watahakikisha Oktoka 29, Dk. Samia ndiye atakayekuwa Rais wa Tanzania na kuwa, sababu ya kufanya hivyo wanayo.

Alisema katika kipindi kifupi cha uongozi wake, amefanya mambo makubwa na ametekeleza ilani ya CCM kwa vitendo pamoja na kuimarisha amani nchini.

Pia, alisema watahakikisha Dk. Mwinyi anapata ushindi wa kishindo kwa upande wa Zanzibar kutokana na mambo makubwa na utekelezaji wa ilani uliotukuka ndani ya kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake.

Previous Post

DK. SAMIA AHIMIZA UPIGAJI KURA OKTOBA 29

Next Post

RAIS DK. SAMIA ATANGAZA OKT. 29 SIKU YA MAPUMZIKO

Next Post
RAIS DK. SAMIA ATANGAZA OKT. 29 SIKU YA MAPUMZIKO

RAIS DK. SAMIA ATANGAZA OKT. 29 SIKU YA MAPUMZIKO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

USAFIRISHAJI MAJINI KUFUNGUA UCHUMI WA MWANZA NA TAIFA

USAFIRISHAJI MAJINI KUFUNGUA UCHUMI WA MWANZA NA TAIFA

2 months ago
UCHAGUZI WA WAJUMBE EALA WAANZA RASMI

UCHAGUZI WA WAJUMBE EALA WAANZA RASMI

2 months ago

Popular News

  • YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    YANGA, SIMBA ZATOA MSIMAMO LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?