• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KUELEKEA DESEMBA 09, POLISI WABAINI MBINU OVU 12

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 4, 2025
in Habari, Kitaifa
0
KUELEKEA DESEMBA 09, POLISI WABAINI MBINU OVU 12

Msemaji wa Jeshi la Polisi, DCP David Misime

0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ELIZABETH JOHN

JESHI la Polisi, limesema limebaini mbinu ovu 12 zilizopangwa na wanaokusudia kuandamana Desemba 09, mwaka huu, yakiwemo matumizi ya silaha za moto.

Aidha, limesema linachukua hatua madhubuti kukabiliana na wimbi la uhalifu wa kimtandao na mipango ya vurugu inayodaiwa kuhamasishwa kupitia mitandao ya kijamii.

Kauli ya Jeshi la Polisi, imekuja siku moja baada ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kuwahakikishia Watanzania, kuwa serikali itaendelea kulinda nchi, mipaka, raia na mali zao wakati wote.

Rais Samia, alitoa kauli hiyo, alipowahutubia Watanzania kupitia mkutano wake na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, (JNICC).

Taarifa ya Polisi iliyotolewa na Msemaji wake, DCP David Misime, imesema Jeshi hilo, linaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kulinda maisha ya wananchi na mali zao, huku likihakikisha amani na utulivu, vinaendelea kuimarika nchini.

 “Hicho wanachohamasisha na kukiita maandamano ya amani, mtu yeyote aliyewasikiliza na akaendelea kuwasikiliza, wanahamasishana na kuelekezana, ambaye hajui kutumia silaha na hajapitia mafunzo, siku hiyo asishike silaha, wawaachie waliopata mafunzo ya matumizi ya silaha. (Kwa maana rahisi, watu hawa wanazo silaha za kutimiza lengo ambalo wamekusudia).

“Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, vimekuwa vikifuatilia kwa karibu sana yanayoendelea katika mitandao ya kijamii na katika makundi sogozi, wakihamasisha wanayoyaita maandamano ya amani yasiyo na kikomo Desemba 9, mwaka huu,” ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa Misime, kupitia mitandao na klabu mbalimbali za mtandaoni, Polisi wamebaini kuwa waandamanaji wanahamasishana siku hiyo kusiwe na shughuli yoyote itakayoendelea na kuhakikisha wanaharibu na kuchoma moto minara ya mawasiliano.

Mengine yaliyobainika, wanahamasishana wahakikishe Bandari ya Dar es Salaam haifanyi kazi, wafunge barabara zote za kuingia na kutoka katika mipaka yote, vijana wakapore mali za watu kwa sababu wanacho kisingizio kwamba, njaa inawasukuma kufanya hivyo na kuzuia huduma zisitolewe hospitalini.

Pia, alisema wanahamasishana kuwafuata walipo watumishi wa serikali kuwadhuru.

“Wapo wengine wameapa na kutamka watakaoandamana wasifike katika mitaa yao, kwani watawashughulikia ipasavyo, wengine wanasema hawatokubali kupata hasara,” alisema.

“Huo ni uhalifu mkubwa unaoendelea kuhamasishwa, hali kama hiyo kwa nchi yoyote duniani, ni tishio kubwa la maisha ya watu, uchumi wa nchi na masuala yote ya kijamii,” alisema.

Hivyo, alisema Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kwa wananchi wote kwa nafasi zao kuepuka wanayoyahamasisha, kwani yamelenga kuharibu taifa na kurudisha machungu na madhara yaliyotokea nyuma.

“Taifa letu linahitaji uponyaji kama jitihada za viongozi wetu wa kitaifa zinavyoendelea kufanyika hivi sasa na hatuhitaji tena vurugu,” alisema.

Kuhusu sherehe za mwisho wa mwaka na mwanzo wa mwaka, Misime alisema Jeshi la Polisi, linawahimiza wananchi waendelee kuzingatia usalama wa maisha na mali zao.

Alisema watakaosafiri kwenda mikoa mbalimbali, wahakikishe wanaacha waangalizi au walinzi katika makazi yao.

Vile vile wazingatie sheria za usalama barabarani na kufuata ishara mbalimbali zilizopo barabarani kuepuka ajali.

Aliongeza kuwa Jeshi la Polisi linawahakikishia wananchi wote wapenda amani, kwamba litaendelea kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, kulinda maslahi ya taifa, maisha ya watu na mali zao.

Previous Post

MKWASA, MTEMI WACHOMBEZA TAIFA STARS

Next Post

RAIS DK. SAMIA AKOSHA VIONGOZI WA KISIASA, DINI

Next Post
RAIS DK. SAMIA AKOSHA VIONGOZI WA KISIASA, DINI

RAIS DK. SAMIA AKOSHA VIONGOZI WA KISIASA, DINI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

ABDULRAZAQ HAMIS BONDIA ANAYECHUKIZWA NA WAAMUZI WANAO PENDELEA WASIO NA UWEZO

ABDULRAZAQ HAMIS BONDIA ANAYECHUKIZWA NA WAAMUZI WANAO PENDELEA WASIO NA UWEZO

5 months ago
MSANII CECY AHIMIZA AMANI

MSANII CECY AHIMIZA AMANI

5 days ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?