• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KIBANO KIKALI WALIOZIMA ‘X-RAY’ TEMEKE

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 25, 2025
in Habari, Kitaifa
0
KIBANO KIKALI WALIOZIMA ‘X-RAY’ TEMEKE
0
SHARES
15
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

SERIKALI imesema imeanza msako dhidi ya watumishi wa afya wanaofanya hujuma na kusababisha wagonjwa wakose huduma ndani ya hospitali za umma na kulazimika kwenda vituo vya binafsi.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, jijini Dar es Salaam, baada ya kubainika vitendo vya kuzima mashine za X-ray katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, hatua iliyosababisha wagonjwa kukosa huduma muhimu na kuelekezwa katika vituo vya binafsi.

Waziri Mchengerwa alisema watumishi wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo watachukuliwa hatua za kisheria bila muhali.

Alisisitiza kuwa serikali haitavumilia hujuma zinazolenga kunufaisha sekta binafsi kwa kuwaumiza wananchi.

Mchengerwa alisema uchunguzi wa awali umebaini baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu walizima mashine za X-ray kwa makusudi, licha ya kuwa vifaa hivyo vya kisasa vinafanya kazi kidijitali ‘Digital X-ray’.

Alisema taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuhusu kuwepo mashine za X-ray zisizofanya kazi katika Hospitali ya Temeke siyo za kweli, bali ni matokeo ya hujuma zilizopangwa.

“Mashine zote za X-ray zilizopo Temeke zinafanya kazi na zimesimikwa kupitia uwekezaji mkubwa wa Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha huduma za afya nchi nzima,” alisema.

Alisema baada ya kupokea taarifa hizo, aliagiza kufanyika kwa uchunguzi wa kina kubaini ukweli.

Uchunguzi uliofanyika ulibaini kuwa hujuma hizo zilisababisha wagonjwa kukosa huduma ndani ya hospitali hiyo na kulazimika kwenda katika vituo binafsi vya afya.

Kwa mujibu wa Mchengerwa, vitendo hivyo ni usaliti mkubwa kwa serikali na wananchi na kwamba uchunguzi unaendelea kuwabaini wahusika wote, iwe ni mtu mmoja au zaidi.

“Natoa onyo kali kwa watumishi wote wa sekta ya afya, yeyote atakayehujumu huduma za afya kwa makusudi atachukuliwa hatua kali za kisheria na kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi na kutopata ajira yoyote ndani ya hospitali, kama ni daktari tutamnyang’anya cheti chake na hatafanya kazi hata nje ya Tanzania,” alisisitiza.

Waziri Mchengerwa aliwahakikishia wananchi kuwa serikali itaendelea kusimamia kwa ukaribu utoaji wa huduma za afya na kuhakikisha vifaa vyote vinavyonunuliwa kwa fedha za umma vinatumika ipasavyo kwa manufaa ya wananchi.

Previous Post

WASOMI, WACHAMBUZI WATOA NENO SERIKALI KUWEZESHA VIJANA

Next Post

‘TUMUOMBEE KARDINALI PENGO’

Next Post
‘TUMUOMBEE KARDINALI PENGO’

‘TUMUOMBEE KARDINALI PENGO’

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MIAKA 64 YA UHURU YAWAIBUA BAYI, RAGE

MIAKA 64 YA UHURU YAWAIBUA BAYI, RAGE

4 months ago
USALITI WA UHUSIANO CHANZO CHA UKATILI

USALITI WA UHUSIANO CHANZO CHA UKATILI

3 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?