• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WASOMI, WACHAMBUZI WATOA NENO SERIKALI KUWEZESHA VIJANA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 25, 2025
in Habari, Kitaifa
0
WASOMI, WACHAMBUZI WATOA NENO SERIKALI KUWEZESHA VIJANA
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ZIANA BAKARI

BAADHI ya wadau wakiwemo wachambuzi wa masuala ya siasa, wasomi, wachumi na viongozi wa dini, wametoa maoni tofauti, kuhusu hatua zinazochukuliwa na serikali kuwawezesha vijana kiuchumi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na UHURU wadau hao walipongeza serikali kuwezesha vijana kiuchumi na kuwatengenezea mazingira bora ya kujiajiri na kuajiriwa.

Katibu mstaafu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Ngemela Lubinga, aliipongeza serikali kwa hatua hiyo kwa sababu inaleta tafsiri nzuri kwamba imejipanga kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana.

Alisema jambo la muhimu vijana wahakikishe wanakuwa na ujuzi utakaowasaidia kupata maarifa mbalimbali ya kuwapa mbinu za kujiajiri.

“Namuunga mkono Waziri Nanauka alichosema kwa sababu serikali ipo kwa lengo la kuwasaidia vijana kufikia malengo yao, niwasihi kukubali kujifunza na serikali isichoke kuwasaidia ,”alisema.

Mwanasiasa ambaye ni mdau wa maendeleo nchini, Abdul Kambaya, alimshauri Nanauka, kufuatilia fedha za mikopo ya vijana inayotolewa na halmashauri.

Alisema utaratibu huo utasaidia sehemu kubwa ya kujua takwimu za vijana waliopata fedha hizo na utendaji kazi wa kila hamshauri utaonekana.

Mtaalamu wa Uchumi, Profesa Samuel Wangwe, aliishauri serikali kuendelea kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana, ambayo itakuwa chachu kupata ujuzi mbalimbali utakaowasaidia kupata kipato cha kujikimu kimaisha.

Katika hatua nyingine, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Dk. Philip Daninga, alisema hatua ya serikali kuwawezesha vijana kiuchumi, italeta tafsiri ya kwamba imetoa kipaumbele zaidi kwa vijana.

Aidha, alibainisha moja ya changamoto kubwa iliyopo ndani ya jamii ni ajira hivyo, serikali imekuja na mwarobaini wa kuunda Wizara ya Vijana ambayo itahakikisha inawawezesha vijana kiuchumi na kijamii.

“Niwashauri vijana kuwa karibu na wizara hiyo kufuatilia fursa mbalimbali zitakazotangazwa wazichangamkie na kuhakikisha wanakuwa na ujuzi utakaowasaidia kujiajiri,”alisema.

Naye, Shekhe wa Wilaya ya Temeke, Zairay Hassan, aliwashauri vijana kuendelea kuiamini serekali kwa sababu jitihada wanazofanya ni kusaidia kuondoa changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana.

Desemba 23, mwaka huu, Nanauka, alisema serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuwawezesha vijana kiuchumi na kijamii, ikiwa ni utekelezaji wa Dira ya Maendeleo 2050 na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Mwaka 2025-2030.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam juzi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka, alisema serikali inalenga kuhakikisha vijana wanapata ajira zenye staha, ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko na fursa za kujiajiri kupitia sekta mbalimbali za uzalishaji.

Alisema Ilani ya CCM, imeweka lengo la kuzalisha ajira zisizopungua milioni nane katika kipindi cha miaka mitano ijayo kupitia kuongeza uzalishaji, kuvutia uwekezaji na kukuza sekta zenye fursa kubwa kwa vijana.

Waziri Nanauka, alitaja changamoto zinazowakabili vijana kuwa ni ukosefu wa ajira, ajira zisizo rasmi na tija, upungufu wa ujuzi na changamoto ya mitaji kwa vijana wajasiriamali na kampuni changa.

Previous Post

RUNGU LA MWIGULU LASHUKA TEMESA

Next Post

KIBANO KIKALI WALIOZIMA ‘X-RAY’ TEMEKE

Next Post
KIBANO KIKALI WALIOZIMA ‘X-RAY’ TEMEKE

KIBANO KIKALI WALIOZIMA ‘X-RAY’ TEMEKE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

MAJALIWA : MRADI GESI YA LNG KUIKOMBOA LINDI KIUCHUMI

7 months ago
WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?