• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

TWIGA STARS YAPEWA MCHONGO WAFCON

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 6, 2025
in Burudani, Michezo
0
TWIGA STARS YAPEWA MCHONGO WAFCON
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

ABDUL DUNIA Na NASRA KITANA

WAKATI michuano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 ikitarajiwa kufanyika mwakani nchini Morocco, wadau mbalimbali wa soka nchini wametoa maoni tofauti nini kifanyike timu ya taifa ya wanawake ‘Twiga Stars’, ifanye vizuri katika fainali hizo kubwa.

Twiga Stars ni miongoni mwa timu 16 zitakazoshiriki katika fainali za WAFCON zitakazofanyika Machi 17 hadi Aprili 3, mwakani.

Timu hizo ni Tanzania, Zambia, Morocco, Malawi, Algeria, Nigeria, Ghana, Burkina Faso, Kenya, Afrika Kusini, Cape Verde, Senegal, Cameroon, Ivory Coast, Mali, Misri.

Hata hivyo katika WAFCON yake hiyo ya tatu katika historia, Twiga Stars haijawahi kutinga hatua ya mtoano, mara zote mbili zilizopita ikiishia makundi na kuburuta mkia.

Katika michuano hiyo, Tanzania imewahi kufuzu mara tatu ikianza hivyo mwaka 2010, 2024 na 2026.

Katika mara yake ya kwanza mwaka 2010, Tanzania iliburuta mkia katika kundi A bila ya pointi ikifungwa mechi zote dhidi ya Afrika Kusini (2-1), Mali (3-2) na Nigeria (3-0).

Pia katika fainali za mwaka 2024, Tanzania iliburuta mkia katika kundi C kwa alama moja, ikifungwa dhidi ya Mali (1-0), Ghana (4-1) na sare ya bao 1-1 dhidi ya Afrika Kusini.

Kuhusu nini kifanyika ili timu hiyo kwa mara ya kwanza itinge hatua ya mtoano, wadau mbalimbali wa soka wametoa maoni tofauti huku wengine wakielekeza macho yao kwa benchi la ufundi.

Mwandishi wa habari za michezo na mchambuzi wa soka la wanawake, Lilian Mukulu, alisema ili Twiga Stars ifanye vizuri ni muhimu wachezaji waandaliwe kisaikolojia na kufanya maandalizi ya mapema.

Alisema WAFCON ni mashindano makubwa hivyo benchi la ufundi la timu hiyo linatakiwa kuboresha mapungufu yaliyojitokeza katika mechi zilizopita kufanya vizuri katika mashindano hayo.

 “Twiga Stars ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri katika mashindano hayo endapo itafanya maandalizi ya mapema kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza, kufanya hivyo kutasaidia timu kuwa na ushindani mkubwa katika kila mchezo,” alisema Lilian.

Naye Salama Ngale ambaye pia ni mchambuzi wa soka la wanawake, alisema Twiga Stars inatakiwa kujipanga vizuri kwani timu inazokwenda kukutana nazo zina ubora mkubwa.

“Ujue ni mashindano makubwa lakini benchi la ufundi linatakiwa kufanya maboresho makubwa ndani ya kikosi chake na pia kuwanoa washambuliaji na mabeki kuwa bora,” alisema Salama.

Akijibu hoja hizo, Kocha wa Twiga Stars, Bakari Shime, alisema atahakikisha anaanza maandalizi mapema kikosi chake kipate muda mzuri wa kufanya mazoezi na kujifunza vitu vingi zaidi.

Alisema kila mchezaji aliyekuwa naye ni bora na yupo tayari kwa mashindano hayo, kwani wanajua ukubwa na umuhimu wa kupambana kupata matokeo mazuri.

“Tunakwenda katika mashindano makubwa, tunatakiwa kufanya maandalizi ya mapema, nitahakikisha timu yangu inaingia kambini mapema na kuanza maandalizi kwa mashindano hayo kwani muda huo utatusaidia kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza katika mechi zilizopita,” alisema Shime.

Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Wanawake Tanzania (TWFA), Somoe Ng’itu, alisema ana imani kubwa timu hiyo itafanya vizuri katika mashindano ya WAFCON mwakani.

 “Sina hofu na kikosi chetu, tunakwenda katika mashindano makubwa kila aliyekuwa katika mashindano hayo ni bora lakini ninaamini timu itafanya vizuri na kuitambulisha vyema nchini yetu,” alisema Somoe.

Katika mechi za kufuzu, Twiga Stars ilianza kwa kuitoa Guinea ya Ikweta katika raundi ya kwanza kwa ushindi wa mabao 4-2 kabla ya kuifunga Ethiopia mabao 3-0.

Previous Post

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA KUANZA MASOMO KWA MKUPUO

Next Post

MATOLA AWAFUNGIA KAZI WASHAMBULIAJI SIMBA SC

Next Post
MATOLA AWAFUNGIA KAZI WASHAMBULIAJI SIMBA SC

MATOLA AWAFUNGIA KAZI WASHAMBULIAJI SIMBA SC

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA BARABARA ZA NDANI KWA KIWANGO CHA LAMI PANGAWE

7 months ago
BIMA YA AFYA YAHITAJI UANDISHI WA HABARI ZA UCHUNGUZI

BIMA YA AFYA YAHITAJI UANDISHI WA HABARI ZA UCHUNGUZI

2 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?