• ePaper
Saturday, May 2, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

JESS NAZ APATA MAJANGA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 13, 2025
in Burudani, Michezo
0
JESS NAZ APATA MAJANGA

MSHAMBULIAJI wa timu ya wanawake ya Tottenham, Jess Naz

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

LONDON, England

MSHAMBULIAJI wa timu ya wanawake ya Tottenham, Jess Naz anatarajia kukaa nje hadi mwishoni mwa msimu huu kufuatia kupata tatizo la goti.

Raia huyo wa England, hataonekana tena katika mechi zote za msimu huu kutokana na tatizo linalomkabili.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25, alipata majeraha katika mchezo kati ya timu yake dhidi ya Aston Villa mwishoni mwa wiki iliyopita na hivyo anatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika goti la kulia.

Taarifa zilizotoka katika mtandao wa klabu zilisema, Jess aliumia goti mara ya pili baada ya kupata tatizo hilo awali na kuukosa msimu wa mwaka 2019-20.

Ilisema Jess ambaye alianza katika kikosi cha kwanza katika mechi zote msimu huu zikiwemo sita za timu ya taifa ya England, hataonekana tena hadi msimu ujao.

“Jess amepata tatizo la goti la kulia ambapo anatarajiwa kuzikosa mechi zote zilizobakia msimu huu.

“Ni pigi kumkosa Jess katika kikosi cha Spurs kwani ni mmoja wa wachezaji muhimu, amekuwa na msaada mkubwa kwa muda mrefu.

“Jess anatarajiwa kufanyiwa upasuaji muda wowote kuanzia hivi sasa kuhakikisha anarejea katika majukumu yake  kama ilivyokuwa awali” ilisema taarifa hiyo.

Wachezaji wengine waliopata tatizo hilo msimu huu ni Michelle Agyemang (Brighton), Maite Oroz (Tottenham), Marie Hobinger (Liverpool), Manu Zinsberger (Arsenal), Sophie Roman Haug (Liverpool), Jill Baijings (Aston Villa) na Katie Reid (Arsenal).

(BBC)

Previous Post

NADO, MASAGALA WATOA NENO STARS

Next Post

KISHINDO CHAANZA AHADI ZA RAIS DK. SAMIA

Next Post
KISHINDO CHAANZA AHADI ZA RAIS DK. SAMIA

KISHINDO CHAANZA AHADI ZA RAIS DK. SAMIA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SMZ KUWACHUKULIA HATUA VIONGOZI AMBAO HAWATAWASILISHA FOMU ZA MAADILI KWA WAKATI

SMZ KUWACHUKULIA HATUA VIONGOZI AMBAO HAWATAWASILISHA FOMU ZA MAADILI KWA WAKATI

5 months ago
MAMBO SAFI BIMA YA AFYA KWA WOTE

MAMBO SAFI BIMA YA AFYA KWA WOTE

4 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?