• ePaper
Friday, June 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

WAZIRI KOMBO NA PROF. KABUDI WAITEMBELEA KAMBI YA TAIFA STARS

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 18, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
WAZIRI KOMBO NA PROF. KABUDI WAITEMBELEA KAMBI YA TAIFA STARS
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHIW ETU

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, wameitembelea Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” iliyokita kambi jijini Cairo nchini Misri.

Waziri Kombo na Profesa Kabudi, wameitembelea kambi hiyo Desemba 17, 2025 na kuikabidhi bendera ya Taifa, ikiwa ni ishara ya kuitakia kila la kheri na kuitia shime kuelekea kwenye kinyang’anyiro cha michuano ya Kombe la AFCON huko nchini Morocco kinachotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwishoni mwa mwaka huu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi Kombo amewasihi vijana hao wachache kati ya wengi wa taifa hili kwa kutanguliza uzalendo kwanza na kuipigania bendera ya Taifa kwa jasho na damu ili kuliletea heshima taifa la Tanzania.

Kwa upande wake, Prof. Kabudi, amekiahidi kikosi hicho ushirikiano wa kila aina katika kuhakikisha kikosi hicho kinafanya vyema katika michuano hiyo mikubwa na yenye heshima kubwa sio tu barani Afrika bali duniani kwa ujumla.

Aidha, Prof. Kabudi amewahimiza Watanzania kuipenda na kuipa moyo timu yao ya Stars kwa kuwashangilia na wale watakao kuwa na nafasi kwenda kujiunga nao kwenye mechi zao zote watakazocheza huko nchini Morocco.

Ikumbukwe kwamba kikosi cha Taifa Stars kipo kundi C lenye timu za Nigeria, Tunisia na Morocco na kikosi hicho kitaanza michuano hiyo kwa kucheza na moja ya timu bora barani Afrika timu ya Taifa ya Nigeria.

Previous Post

MAGAMBO AAHIDI KUENDELEZA MAFANIKIO YA PSSSF

Next Post

BALOZI KUSILUKA ATAKA TAARIFA POTOFU ZIJIBIWE

Next Post
BALOZI KUSILUKA ATAKA TAARIFA POTOFU ZIJIBIWE

BALOZI KUSILUKA ATAKA TAARIFA POTOFU ZIJIBIWE

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MSANII CECY AHIMIZA AMANI

MSANII CECY AHIMIZA AMANI

3 months ago
KATIBUBMkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), BalozibDk. Asha-Rose Migiro

CCM IMEJIPANGA KUFANYA KAMPENI ZA KISTAARABU – BALOZI DK. MIGIRO

10 months ago

Popular News

  • SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL-NINO

    SERIKALI YAZITAKA TAASISI ZOTE KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL-NINO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SAMAMBA AWAFUNDA WAKAGUZI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RUNGU ZITO KUWASHUKIA WAWEKEZAJI ‘JANJAJANJA’

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA KAZI KAZI UBINGWA LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, AZAM FC HAIJAISHA HADI IISHE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?