MOROCCO
MACHO ya mashabiki yapo kuwaangalia nyota mbalimbali watakaoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025).
Michuano hiyo imepangwa kuanza kufanyika Jumapili katika viwanja mbalimbali nchini Morocco.
Mchezaji Achraf Hakimi wa Morocco ni nyota ambaye anasubiriwa kuangaliea vitu atakavyovifanya ndani ya dimba.
Mohamed Salah wa Misri hii inaweza kuwa ‘ngoma ya mwisho’ ya mchezaji huyo kupata kombe moja ambalo litaweka historia na wengi wanataka kuona atang’ara asu vinginevyo.
Tayari mchezaji huyo amekuwa anahusishwa kuondoka Liverpool na kwenda kucheza Ligi Kuu ya Saudi Arabia.
Victor Osimhen wa Nigeria ni staa mwingine ambaye utimamu wake humfanya kuwa ndoto mbaya kwa mlinzi yeyote kutokana na uwezo wake kuwa mkubwa wa kupachika mabao.
Brahim Díaz wa Morocco ni mchezaji wa Real Madrid ameongeza mwelekeo mpya wa ubunifu katika safu ya kiungo ya Morocco.
Mchezaji mwingine ni Ademola Lookman wa Nigeria ambaye amekuwa shujaa ndani ya kikosi cha nchi hiyo katika maeneo magumu anapokuwa dimbani.
Omar Marmoush wa Misri ni mshambulizi anayeichezea timu ya Manchester City kwa sasa ni mmoja wa washambuliaji walio katika kiwango bora zaidi duniani.




