RABAT, Morocco
MICHUANO ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ilianza kutimua vumbi juzi jijini Rabat, Morocco.
Katika michuano hiyo inayoshirikisha timu 24 kutoka Afrika, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa kushirikiana na mwenyeji Morocco, wameandaa maeneo mbalimbali kwa mashabiki kuhakikisha wanapata burudani ya kutosha katika michuano hiyo.
Maelfu ya mashabiki hujitokeza katika maeneo hayo kabla ya kwenda uwanjani, baada au wengine huamua kutokwenda uwanjani bali hubakia kutazama mpira kwa televisheni katika maeneo hayo.
Maeneo hayo maarufu Fan Parks ni sehemu muhimu kwa mashabiki kufurahia burudani mbalimbali ikiwemo muziki na maeneo ya kununua jezi na vitu mbalimbali vya soka na utamaduni.
MAENEO YA MASHABIKI AFCON MOROCCO
Rabat: Esplanade OLM Souissi
Rabat: Sale Bab El Mrissa
Casablanca: Espace Toro
Casablanca: Espace Météo
Agadir: Agadir Beach (La Marina)
Fes: Jardin Botanique
Marrakech: Bab Jdid
Tangier: Villa Harris Park




