RABAT, Morocco
MSHAMBULIAJI wa timu ya taifa ya Gabon, Denis Bouanga amesema wana matumaini ya kuweka historia ya aina yake katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) inayoendelea nchini Morocco.
Bouanga ni mmoja wa wachezaji wenye uzoefu mkubwa katika michuano hiyo ndani ya kikosi cha Gabon msimu huu.
Amesema mipango yake ni kuisaidia Gabon kufanya vyema katika michuano ya AFCON msimu huu japokuwa watakutana na upinzani mkali.
“Nina matumaini nitaisaidia timu kufika hatua mbali katika michuano ya AFCON japokuwa tutakutana na upinzani mkubwa.
“Tunataka kufika mbali na kuwa na mafanikio ambayo hatujawahi kuyapata hapo awali katika michuano ya AFCON,” alisema.
(BBC)




