• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

SIMBACHAWENE AZINDUA NAMBA YA KUFUATILIA NIDA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 30, 2025
in Habari, Kitaifa
0
SIMBACHAWENE AZINDUA NAMBA YA KUFUATILIA NIDA
0
SHARES
12
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, amezindua namba maalumu, itakayotumiwa na wananchi kufuatilia Kitambulisho cha Taifa baada ya kuwasilisha maombi ya kitambulisho.

Hatua hiyo itatoa fursa kwa wananchi kupata na kujua taarifa za maombi ya kitambulisho kwa kutumia namba hiyo maalumu.

Waziri huyo alizindua namba hiyo maalumu Dar es Salaam, ambapo alisema vitambulisho vingi vimezalishwa na tayari vimepelekwa sehemu husika zikiwemo wilayani.

“Hivi leo tunavyozungumza katika wilaya zetu zote nchini, viko vitambulisho vingi sana ambavyo havijachukuliwa na sababu kubwa mwombaji hajui kitambulisho chake kipo katika hatua gani

“Kupitia mfumo huu ambao ninauzindua, utajibiwa na utaambiwa kama namba yako umepata ndani ya siku tano na kama hujapata ndani ya siku tano tangu ulipoomba ukitumia mfumo huu (15274) utajibiwa kwanini hujapata,”alisema Waziri Simbachawene.

Aliongeza pia serikali inafikiria kusitisha matumizi ya namba ya utambulisho (NIN), kwasababu watu wengi wameacha kwenda kuchukua vitambulisho.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), James Kaji, alisema mamlaka imeendelea kushusha vitambulisho hadi ngazi ya kata, lakini bado wananchi hawajavifuata kabla ya kuvipeleka wilayani.

Alisema baada ya kuvipeleka wilayani, anaamini kupitia mfumo huo mpya wa namba 15274, vitambulisho vitaendelea kufuatwa kwa kuwa umerahisisha zaidi taarifa za mwombaji kupitia simu ya mkononi.

Previous Post

DK. MWIGULU ASHUSHA PRESHA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI

Next Post

PM MWIGULU KUVALIA NJUGA MIGOGORO YA ARDHI

Next Post
PM MWIGULU KUVALIA NJUGA MIGOGORO YA ARDHI

PM MWIGULU KUVALIA NJUGA MIGOGORO YA ARDHI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA ANAVYOTAFSIRI ‘KAZI NA UTU’ KWA VITENDO

DK. SAMIA ANAVYOTAFSIRI ‘KAZI NA UTU’ KWA VITENDO

7 months ago
ROONEY KUREJEA MAN UNITED

ROONEY KUREJEA MAN UNITED

3 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?