• ePaper
Friday, January 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. SAMIA ATEUA, ATENGUA VIGOGO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 8, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DK. SAMIA ATEUA, ATENGUA VIGOGO
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi na kutengua viongozi mbalimbali ambapo aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene na Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC) Profesa  Eliakimu Zahabu, uteuzi wao umetenguliwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka kisha kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu ilisema Patrobas Katambi ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Kabla ya uteuzi huo, Katambi alikuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, akichukua nafasi ya Simbachawene ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Pia, taarifa hiyo ilisema Profesa Palamagamba Kabudi ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum). Kabla ya uteuzi huo, Profesa Kabudi alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Vilevile, taarifa hiyo ilieleza kuwa Paul Makonda ameteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambapo kabla ya uteuzi huo, Makonda alikuwa Naibu waziri katika wizara hiyo.

Kadhalika, Dennis Londo ameteuliwa kuwa Naibu Waziri, Viwanda na Biashara ambapo kabla ya uteuzi huo Londo alikuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Taarifa hiyo ilibainisha kuwa Ayoub Mohamed Mahmoud ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Richard Muyungi ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) akichukua nafasi ya Mhandisi Cyprian Luhemeja ambaye ameteuliwa kuwa balozi.

Aidha, Mhandisi Zena Ahmed Said ameteuliwa kuwa Balozi, Waziri Salum ameteuliwa kuwa Balozi, Meja Jenerali Mbaraka Mkeremy ameteuliwa kuwa Balozi huku Mhandisi Ally Samaje ameteuliwa kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST).

Mhandisi Samaje anachukua nafasi ya Dk. Mussa Daniel Budeba huku uteuzi wa Profesa Eliakimu Zahabu, Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (NCMC) umetenguliwa.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa uapisho wa viongozi wateule utafanyika Januari 13 mwaka huu, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma kuanzia saa 8.00 mchana.

Previous Post

DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

Next Post

TASAF ILIVYOCHOCHEA KILIMO, KUBADILI MAISHA YA WANANCHI

Next Post
TASAF ILIVYOCHOCHEA KILIMO, KUBADILI MAISHA YA WANANCHI

TASAF ILIVYOCHOCHEA KILIMO, KUBADILI MAISHA YA WANANCHI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WASIRA : DK. SAMIA ANASTAHILI ‘MITANO TENA’

WASIRA : DK. SAMIA ANASTAHILI ‘MITANO TENA’

4 months ago
BIL. 36.6/- ZAPAISHA UCHUMI WA VIJANA

BIL. 36.6/- ZAPAISHA UCHUMI WA VIJANA

2 weeks ago

Popular News

  • MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

    MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KATIBU MKUU CCM AWATAKA WANACHAMA KUSHIRIKI KIKAMILIFU VIKAO VYA MASHINA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TASAF ILIVYOCHOCHEA KILIMO, KUBADILI MAISHA YA WANANCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA ATEUA, ATENGUA VIGOGO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MIGIRO AJA KIVINGINE CCM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?