• ePaper
Tuesday, May 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MRADI WA BILIONI 18.9/- BUKOBA WAMPA SIFA RAIS DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 26, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MRADI WA BILIONI 18.9/- BUKOBA WAMPA SIFA RAIS DK. SAMIA
0
SHARES
13
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na CELINA MATHEW

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa juhudi zake za kufanikisha utekelezaji wa mradi wa soko la kisasa na stendi ya mabasi mkoani Bukoba, uliokuwa ukisubiriwa kwa zaidi ya miaka 10, lakini sasa unaendelea kutekelezwa ndani ya kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, alipofanya ukaguzi wa mradi huo wenye thamani ya Sh bilioni 18.9.

Amesema utekelezaji wa mradi huo unaonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kutimiza ahadi kwa wananchi, akibainisha kuwa fedha zinazotumika ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na si msaada wa bure, jambo linalodhihirisha uwajibikaji katika matumizi ya rasilimali za maendeleo.

Aidha, Kihongosi amesema ameridhishwa na ubora wa ujenzi unaoendelea, huku akiwapongeza wahandisi, mkandarasi pamoja na vijana wanaoshiriki katika utekelezaji wa mradi huo.

Amesisitiza umuhimu wa kulipwa kwa stahiki za wafanyakazi kwa wakati na kuhimiza kuongeza kasi ya ujenzi licha ya changamoto za mvua.

Kwa upande wake, Msimamizi wa mradi huo, Nixon Kissa, amesema utekelezaji umefikia asilimia 19.45 na unatarajiwa kukamilika mwaka 2027.

Ameeleza kuwa mradi huo utakuwa na vizimba 1,848 pamoja na maduka 234, hatua itakayochochea ukuaji wa biashara katika mkoa wa Kagera hususan Bukoba.

Kwa upande wake, Msimamizi wa mradi huo, Nixon Kissa, amesema utekelezaji umefikia asilimia 19.45 na unatarajiwa kukamilika mwaka 2027.

Ameeleza kuwa mradi huo utakuwa na vizimba 1,848 pamoja na maduka 234, hatua itakayochochea ukuaji wa biashara katika mkoa wa Kagera hususan Bukoba.

Previous Post

PBPA YAAGIZWA KUHARAKISHA UPOKEAJI NA USAZAMBAZAJI WA MAFUTA NCHINI

Next Post

RUFANI YA SENEGAL KUSIKILIZWA

Next Post
RUFANI YA SENEGAL KUSIKILIZWA

RUFANI YA SENEGAL KUSIKILIZWA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

UKILA BATA KRISMASI, USISAHAU ADA JANUARI

5 months ago
MAKOCHA YANGA, SIMBA WAZITAMBIA  AL AHLY, ESPERANCE

MAKOCHA YANGA, SIMBA WAZITAMBIA  AL AHLY, ESPERANCE

4 months ago

Popular News

  • MWIGULU AKERWA WANAOPORA HAKI

    MWIGULU AKERWA WANAOPORA HAKI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA YATAKA WAANDISHI KUHAMASISHA WAAJIRI KURIPOTI MATUKIO WCF

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAKONDA ASISITIZA KULINDWA KWA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA CHINA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?