• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

NYOTA YANGA WAPEWA TANO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 10, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
NYOTA YANGA WAPEWA TANO
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

KOCHA wa Yanga, Pedro Goncalves, amewapongeza wachezaji wake kwa kuonyesha kiwango kikubwa katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Pamba Jiji ambao kikosi hicho kilishinda 3-0.

Yanga ilicheza mechi hiyo juzi katika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza ambapo miamba hiyo ilipata mabao yake kupitia kwa Mudathir Yahya aliyepachika mawili na Maxi Nzengeli.

Kocha Pedro alisema amefurahishwa na kiwango walichokionyesha wachezaji wake, lakini bado ana kazi ya kuboresha maeneo mbalimbali katika mechi zijazo.

Alisema kila mchezaji alionyesha uwezo mkubwa hatua ambayo imechangia kuondoka na pointi tatu muhimu.

“Tumeshinda na kupata pointi tatu, lakini niseme tu ukweli ni ngumu sana kucheza katika Uwanja wa CCM Kirumba, ila niwapongeze wachezaji wangu kwa kiwango kikubwa walichokionyesha kuhakikisha tunapata matokeo mazuri,” alisema Pedro.

Kocha huyo alisema ushindi huo wanauelekeza kwa mashabiki wao kutokana na sapoti kubwa wanayowaonyesha kuhakikisha wanashinda katika kila mchezo.

Naye Kocha wa Pamba Jiji, Francis Baraza alisema haelewi ni kitu gani kimewapata wachezaji wake hadi kuwa “wazito” kiasi cha kushindwa kufuata maelekzo na mpango kazi wa kiufundi waliokubaliana.

Alisema pamoja na ubora wa wapinzani, wachezaji wake wameshindwa kufuata kile ambacho amewafundisha.

“Kwa sasa nina kazi kubwa ya kwenda kufanya kurekebisha mapungufu yaliojitokeza katika mchezo huo, tunahitaji kupata ushindi katika mechi zinazofuata,” alisema.

Katika msimamo wa ligi hiyo, Yanga ipo kileleni ikiwa na pointi 44 huku Pamba Jiji ikishika nafasi ya sita kwa pointi 26 katika michezo 18.

Previous Post

TUMAINI JIPYA LA MIKOPO KWA VIJANA

Next Post

KOCHA SIMBA ACHEFUKWA

Next Post
KOCHA SIMBA ACHEFUKWA

KOCHA SIMBA ACHEFUKWA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

DK. SAMIA AMELETA MIRADI MIKUBWA LINDI – MAJALIWA

8 months ago
MANNY PACQUIAO KUTUA BONGO NA MAMBO MAWILI

MANNY PACQUIAO KUTUA BONGO NA MAMBO MAWILI

3 months ago

Popular News

  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL. 195.66/- KUJENGA BONDE MTO MSIMBAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULEGA AJIBU MAPIGO KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NEEMA YAJA, MIKAKATI HADHARANI KUINUA VIJANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?