• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

ASKOFU MNDOLWA: TUME YA JAJI CHANDE ITAIPELEKA NCHI PAZURI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 14, 2026
in Habari, Kitaifa
0
ASKOFU MNDOLWA: TUME YA JAJI CHANDE ITAIPELEKA NCHI PAZURI
0
SHARES
2
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

ASKOFU Mkuu wa Kanisa Anglikana nchini, Dk. Mahimbo Mndolwa, amesema Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29, itaipeleka nchi pazuri.

Kauli hiyo aliyoitoa Dar es Salaam,  imekuja kipindi ambacho Tume ya Kuchunguza Matukio Kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu, ikiendelea na kazi zake katika hatua ya mwisho.

Askofu huyo Mkuu wa Kanisa Anglikana, Dk. Mndolwa, alisema Tume hiyo imeonesha mwanga kuwa tunakwenda mahali sahihi.

Dk. Mndolwa alifafanua katika vikao vyake vya Umoja wa Mataifa, amekuwa akieleza Tanzania haijafikia hatua ya kuomba nguvu za nje katika kutatua matatizo yake, kwa kuwa imekuwa ikichukua hatua.

“Ukweli kwa aina ya watu tulio nao mle ndani ya Tume, tunaamini tunaelekea mahali sahihi na kujenga taifa sahihi zaidi,” alisema Askofu Dk. Mndolwa.

Alisema, hata katika maandiko ya Mungu yanasisitiza umuhimu wa ndugu kutatua matatizo yao wenyewe kwanza kabla ya kueleza au kutafuta suluhu kwa watu wa nje.

Akifafanua mantiki ya maandiko hayo akihusisha na Tume, Askofu Dk. Mndolwa alisema hatua ya Tanzania kufanya uchunguzi ni uthibitisho kuwa Tanzania imeamua kutafuta ufumbuzi wa matatizo yake ya ndani yenyewe.

“Ukweli, hata katika maandiko ya dini tunaelezwa ndugu yako akikukosea unakwenda  kuzungumza naye. Kama hakukusikia ndipo utaenda kueleza Kanisa, ” alifafanua Askofu Dk. Mndolwa.

Alisema hatua ya Tanzania kujichunguza imeonyesha ukomavu mkubwa, ambao umekuwa ukifanyika kwa nyakati tofauti na kwa miaka mingi.

“Tumefanya hivi kwa miaka mingi sana. Hatukwenda huko nje kupiga parapanda. Tutapiga parapanda tutakapoona tumeshindwa,” alisema.

Dk. Mndolwa alisema hatua hiyo pia inaonesha Tanzania ni huru huku akisisitiza, inapokea maoni kutoka nje lakini haiwezi kuyakimbilia.

“Mawazo kutoka nje tutayasikiliza ila hatuwezi kuyakimbilia. Mimi mwenyewe ni mjumbe wa Kanisa Anglikana katika UN, wanatuuliza ninyi Watanzania mbona hamtukaribishi. Tuna wajibu bado tunaweza kuongea wenyewe,” alisisitiza.

Dk. Mndolwa alimpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuunda Tume hiyo chini ya Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Chande, itafute kwanza suluhu ya ndani.

Dk. Mndolwa alisema Tume huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Vurugu zilizotokea kabla na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka jana inaonesha mwanga kuwa tunakwenda mahali sahihi.

Previous Post

WASHIRIKI MISS WORLD TANZANIA WAPEWA SOMO

Next Post

DCEA YAKAMATA SHEHENA YA MIRUNGI KUTOKA KENYA, YAKAMATA BOTI BAGAMOYO

Next Post
DCEA YAKAMATA SHEHENA YA MIRUNGI KUTOKA KENYA, YAKAMATA BOTI BAGAMOYO

DCEA YAKAMATA SHEHENA YA MIRUNGI KUTOKA KENYA, YAKAMATA BOTI BAGAMOYO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : TUTAKAMILISHA BANDARI YA UVUVI KILWA

DK. NCHIMBI : TUTAKAMILISHA BANDARI YA UVUVI KILWA

6 months ago
KIHONGOSI ATOA MAAGIZO KWA MADIWANI 

KIHONGOSI ATOA MAAGIZO KWA MADIWANI 

4 months ago

Popular News

  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NYAMBUI AFUNGUKAAMANI KATIKA MICHEZO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, MBEYA CITY KAZI IPO LEO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AFICHUA KUWA NA KIPAJI CHA SOKA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?