• ePaper
Wednesday, April 22, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 22, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA
0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU

MAKAMU wa Rais, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema taifa litaukumbuka mchango mkubwa alioutoa marehemu Askofu Bernadin Mfumbusa, enzi za uhai wake ukiwemo kuwa kiungo muhimu wa Kanisa Katoliki na dini zingine.

Balozi Dk. Nchimbi alisema hayo, baada ya kushiriki ibada ya kumuaga na kumwombea Askofu wa Jimbo Katoliki Kondoa, Mfumbusa, iliyofanyika Katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Paulo wa Msalaba , Jimbo Kuu Katoliki Dodoma.

Alisema Askofu Mfumbusa alijitolea katika kuunganisha dini na madhehebu zifanye kazi kwa kuheshimiana, kushirikiana na kupendana.

Kwa mujibu wa Balozi Dk. Nchimbi, taifa litakumbuka mchango wake katika kuhamasisha elimu, kusimamia ujenzi na uendelezaji wa huduma za afya wilayani Kondoa na taifa kwa ujumla.

Makamu wa Rais alisema Askofu Mfumbusa alitoa mchango katika sekta ya mawasiliano na habari, akiwa mbobezi na mwalimu katika fani hiyo.

Nchimbi alisema Askofu Mfumbusa atakumbukwa kwa kutimiza wajibu wake kwa binadamu, kwa kutambua maisha ya kutimiza wajibu kwa Mungu.

SALAMU ZA RAIS

Pia, Balozi Dk. Nchimbi aliwasilisha salamu za pole za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, alizotoa kwa kanisa, waumini na familia na kuiombea familia nguvu na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Makamu wa Rais aliwashukuru viongozi wa Kanisa Katoliki kwa malezi ya Askofu Mfumbusa ambayo yalimfanya kuwa mtume wa taifa zima.

IBADA

Ibada hiyo, iliongozwa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, Mhashamu Wilbroad Kibozi na kuhudhuriwa na maaskofu mbalimbali, mapadre, watawa, viongozi  wa serikali na wananchi.

Previous Post

SITAWAANGUSHA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MPINA APIGWA ‘STOP’ URAIS ACT-WAZALENDO

MPINA APIGWA ‘STOP’ URAIS ACT-WAZALENDO

8 months ago
TAKUKURU YAFUNGUA MASHAURI MATATU YA UHUJUMU UCHUMI SIHA

TAKUKURU YAFUNGUA MASHAURI MATATU YA UHUJUMU UCHUMI SIHA

2 months ago

Popular News

  • DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

    DK.NCHIMBI AMTAJA ASKOFU MFUMBUSA NGUZO YA UMOJA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SITAWAANGUSHA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA YATIMUA VUMBI CAF, SIMBA MMH

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AMPA TANO SIMBU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAAJABU YA DP WORLD SIKU 730 BANDARINI DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?