Na NASRA KITANA
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF), limesema limeridhishwa na kiwango cha cha maandalizi yanayofanywa na Tanzania, kw ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2027).
Tanzania itaandaa fainali hizo pamoja na Kenya na Uganda, kuanzia Juni 19 hadi Julai 17, 2027.
Pamoja na pongezi hizo, CAF imeitaka kamati ya maandalizi kuongeza kasi ya utekelezaji wa miundombinu ambayo haijakamilika katika kipindi cha miezi tisa iliyosalia, kabla ya kuanza mashindano.
Rais wa CAF, Rais wa CAF, Patrice Motsepe, aliyasema hayo, jijini Dar es Salaam jana, alipofanya ziara na kukagua Uwanja wa Benjamin Mkapa, ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa maandalizi ya fainali hizo nchini.
Motsepe alisema ameona kasi ya maandalizi kwa Tanzania na anaimani kuwa wiki chache kabla ya kuanza mashindano, kila kitu kitakuwa kimekamilika.
“Nimefurahi kuona kasi ya Tanzania, maandalizi yapo katika hatua nzuri na nina imani yatakamilika kwa wakati, sehemu ambapo kasi ni ndogo naamini itaongezwa na kukamilika kwa wakati,” alisema Motsepe.
Alisema CAF inatarajia kuona maeneo ambayo yameonekana kuwa nyuma katika maandalizi yataharakishwa na kurekebishwa, nina imani kubwa zaidi baada ya kupokea ripoti ya kina kuhusu maendeleo ya Tanzania.
Aliongeza kuwa anatarajia kurejea nchini Januari 2027 kwa ajili ya kufanya tathmini ya mwisho, kabla ya mashindano kuanza.
Ziara ya Motsepe imekuja wakati Tanzania ikiendelea kufanya maandalizi kwa kasi na kufikia asilimia 80,
Uwanja wa Benjamin Mkapa ulifungwa Machi 2026 na kufanyiwa maboresho ya mwisho ya eneo la kuchezea.




