• ePaper
Sunday, June 7, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MOROGORO YA DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
August 30, 2025
in Habari, Siasa, Uchaguzi
0
MOROGORO YA DK. SAMIA
0
SHARES
19
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Morogoro

WANANCHI mkoani Morogoro wamethibitisha kwa vitendo kiu yao kuendeleza rekodi ya kuongoza kitaifa kwa kura za Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu, baada ya kumhakikishia mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kumpigia kura za kishindo.

Hilo limethibitika katika mkutano wa kampeni za Urais uliofanyika leo (Agosti 29 mwka huu) viwanja vya Tumbaku mkoani Morogoro ambapo maelfu ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo maarufu kwa shughuli za kilimo kujitokeza kumuunga mkono Dk. Samia alipokuwa akinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambapo ameahidi kuurejesha mkoa huo kuwa wa viwanda.

Msafara wa Rais Dk. Samia uliwasili katika viwanja hivyo saa 14:42 mchana, ukisindikizwa na msafara wa matarumbeta, pikipiki huku nyimbo maalum ya kumpokea ikipigwa na bendi ya Tanzania One Theatre (TOT).

Akihutubia mkutano huo, Dk. Samia alisema CCM imejipanga vyema kuleta mageuzi makubwa katika mkoa huo.
Alisema katika miaka mitano ijayo, serikali itawekeza zaidi katika sekta ya afya kwa kujenga vituo vya afya 28 na zahanati 97 huku Manispaa ya Morogoro vitajengwa vituo viwili vya afya na zahanati 11.

Pia, alisema serikali itakamilisha maabara, jengo la upasuaji na Kituo cha Afya Tungi pamoja na wodi ya mama na mtoto eneo la Mafiga.


“Tuawekeza katika elimu kwa kujenga madarasa 190 kwa shule za sekondari, ujenzi wa shule mpya ya wenye mahitaji maalum na kuendeleza sera ya elimu bila ada.

“Tutafikisha umeme vitongoji vyote na kuhamasisha uunganishaji umeme kwenye kaya. Tutajenga soko la kisasa Morogoro mjini kwa ajili ya wajasiriamali na wamachinga ili kuboresha mazingira yao.

Aliongea: “Tutajenga masoko mengine wilaya za Kilosa na Malinyi, kuwekeza kwenye mbolea ya ruzuku na mbegu bora. Tutajenga maghala matano wilayani Kilosa katika ushoroba wa reli ya SGR kurahisha usafirishaji mazao.”

Kadhalika, alisema CCM kupitia ilani yake imepanga kujenga vituo vya kupoza umeme, Tungi, Msavu, Kilosa na Mvomero.
“Dhamira yetu ni kuufufua Mkoa wa Morogoro kuwa Mkoa wa viwanda, viwanda vipya vinakuja vikubwa na vidogo. Jitihada hizo zitasaidia kuvutia uwekezaji na hivyo kuongeza fursa za ajira,” alieleza.

Previous Post

CCM IMEJIPANGA KUFANYA KAMPENI ZA KISTAARABU – BALOZI DK. MIGIRO

Next Post

TANZANIA IPO SALAMA MIKONONI MWA CCM – PETER MSIGWA  

Next Post
TANZANIA IPO SALAMA MIKONONI MWA CCM – PETER MSIGWA  

TANZANIA IPO SALAMA MIKONONI MWA CCM – PETER MSIGWA  

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON

SERIKALI YAWATAKA WATANZANIA KUCHANGAMKIA FUSRA AFCON

9 months ago
DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

DK. MWINYI : YAJAYO YANAFURAHISHA KASKAZINI UNGUJA

9 months ago

Popular News

  • MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    MWANZA KINARA USIMAMIZI MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WFP KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA USIMAMIZI WA MAAFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • HESHIMA KUBWA KWA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWIGULU: MAMBO MAZURI YANAKUJA, AIPA TANO SERENGETI BOYS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERENGETI BOYS HESHIMA KILA KONA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?