• ePaper
Wednesday, September 9, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

GAVU ATAJA SIFA ZA NAFASI URAIS, UBUNGE, UDIWANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 29, 2025
in Habari, Kitaifa
0
Katibu wa Idara ya Organaizesheni ya CCM, Issa Haji Gavu
0
SHARES
14
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

 Na NJUMAI NGOTA,

Mwanza

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema nafasi za urais, ubunge na udiwani zinahitaji watu wenye utayari, uwezo, dhamira, malengo na kusudio la kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa mkoani hapa na Katibu wa Idara ya Organaizesheni ya CCM, Issa Haji Gavu, alipozungumza katika mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM zilizofanyika viwanja vya Furahisha, wilayani Nyamanga.

Mgombea Mwenza wa Urais kupitia CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, alizindua kampeni za uchaguzi mkoani humo.

Gavu amesema Chama kinaheshimu nafasi ya kiongozi ya kukiwakilisha.

“Nafasi ya kiongozi wa kuiwakilisha jamii yetu, tunaamini nafasi za uongozi iwe udiwani, ubunge na urais ni nafasi ambazo zinahitaji watu wenye utayari, uwezo, dhamira, malengo na wenye kusudio la kusukuma mbele gurudumu la maendeleo,”amesema.

Amesema yapo mambo ambayo yanabahatishwa, kwa jambo la uongozi wa taifa, majimbo na kata siyo ya fahari, hivyo wanahitaji viongozi wa kulitoa taifa lilipokuwepo jana, leo na kesho.

Gavu alisema hakuna kiongozi wa chama kingine chochote mwenye kujua dhamira hiyo, zaidi ya viongozi wanaotokana na CCM.

Amewaomba wananchi vyama vingine vitakapokuja wavipe nafasi ya kuvisikiliza, wapime na kutazama dhamira zao.

“CCM imejiandaa kwa sera, Ilani na kwa kutambua yapo mafanikio tuliyofanikiwa, zipo changamoto tunazokabiliana nazo na ipo mipango ya kuachana na changamoto hizo.

“Tutakapokuja kwenu, hatuji kulalamika, tutakuja kuwaeleza tumetoka wapi, tupo wapi na tunakwenda wapi, hiyo ni dhamira ya Chama,”amesema.

Previous Post

DK. SAMIA, BALOZI NCHIMBI WAAHIDIWA KURA ZA KISHINDO

Next Post

YANGA, SIMBA MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Next Post
Wachezaji wa SIMBA na YANGA

YANGA, SIMBA MECHI YA KISASI NA HESHIMA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAZIRI MKUU ARIDHISHWA UJENZI BANDARI YA UVUVI KILWA

WAZIRI MKUU ARIDHISHWA UJENZI BANDARI YA UVUVI KILWA

9 months ago
DEMOKRASIA ISIZICHAFUE NCHI ZETU – RAIS DK. SAMIA

DEMOKRASIA ISIZICHAFUE NCHI ZETU – RAIS DK. SAMIA

4 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    RAIS DK. SAMIA, NDEJEMBI TURUFU YA MAENDELEO KWA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI AONYA, ATOA SIKU 60 WENYE SILAHA HARAMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NDEJEMBI MZIGONI RASMI, AKEMEA KAZI KWA MAZOEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUME MIPANGO, NIRC WAJADILI UBORA MIRADI YA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASAUNI AANIKA UMAHIRI WA TANZANIA INAVYOLINDA UDONGO, MATUMIZI MBOLEA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?