• ePaper
Wednesday, October 15, 2025
Subscribe
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
No Result
View All Result
Home Habari

GAMONDI ALIA NA MUUNGANIKO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 8, 2025
in Habari, Kitaifa, Michezo
0
GAMONDI ALIA NA MUUNGANIKO
0
SHARES
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

LICHA ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi ya Kenya katika Kombe la Kagame, Kocha wa Singida Black Stars, Miguel Gamondi, amesema bado kikosi chake hakina muunganiko mzuri.

Singida ilipata ushindi huo katika mchezo wake wa pili wa michuano hiyo uliopigwa katika Uwanja wa KMC jijini Dar es Salaam.

Awali, miamba hiyo ilitoka suluhu ilipovaana na Ethiopia Coffee ya nchini Ethiopia.

Gamondi alisema kutokana na muda mfupi aliokuwa nao tangu ajiunge na timu hiyo, wachezaji bado hawajafikia muunganiko anaoutaka.

Kocha huyo alikiri kwamba kuna wakati wanashindwa kudhibiti mchezo kutokana na wachezaji wake kutozoeana vya kutosha, jambo linalosababisha makosa ya mara kwa mara uwanjani.

“Tumepata ushindi lakini sijapata muunganiko ndani ya kikosi changu, nitaendelea kupambana kuijenga timu iweze kuwa vile ambavyo ninahitaji,” alisema.

Kocha huyo alisema kwamba kadri siku zinavyosonga na wachezaji wakipata mechi zaidi za ushindani, changamoto hizo zitapungua na timu itaonekana bora zaidi.

Wakati huo huo, Gamondi alisema katika mechi mbili zilizopita za mashindano ya Kagame, alikosa huduma za wachezaji wake muhimu akiwemo Khalid Aucho na Marouf Tchakei.

Wachezaji hao kwa mujibu wake wana mchango mkubwa katika kuongeza nguvu na ubora wa kikosi hicho na kurejea kwao kutakuwa na maana kubwa katika malengo ya timu.

Naye kocha wa Polisi Ettiene Ndayiragije alikiri kwamba kuna wakati wanashindwa kudhibiti mchezo kutokana na wachezaji wake kutozoeana vya kutosha, jambo linalosababisha makosa ya mara kwa mara uwanjani.

Alisema kadri siku zinavyosonga na wachezaji wakipata mechi zaidi za ushindani, changamoto hizo zitapungua na timu itaonekana bora zaidi.

“Kikosi changu kimeleta somo baada ya kupoteza mchezo huo hivyo tunakwenda kujipanga upya tupate ushindi katika mchezo unaofuata,” alisema.

Ndayiragije alisema wapinzani wao ni timu yenye uzoefu mkubwa na waliweza kudhibiti mchezo hata walipokuwa chini ya presha.

Previous Post

MBAPPE AMFIKIA HENRY UFARANSA

Next Post

CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

Next Post
CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

CHAMA MENO NJE SINGIDA BLACK STARS

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

2 days ago

Uchumi wa Tanzania unaendelea kukua kwa asilimia 6.8

2 months ago

Popular News

  • SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    SIMBA NI MWENDO WA MABAO LIGI KUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • JESCA: DK. SAMIA NI KIONGOZI JASIRI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA WATANZANIA YAKO KATIKA MATENDO – DK. MIGIRO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWINYI AAHIDI KUJENGA HOSPITALI MAALUMU YA SARATANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
error: Content is protected !!
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2025 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.