• ePaper
Monday, May 25, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. BASHIRU AELEZEA UJASIRI WA DK. SAMIA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 11, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
DK. BASHIRU AELEZEA UJASIRI WA DK. SAMIA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MUSSA YUSUPH,

Singida

KATIBU Mkuu Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ali, amefunguka kuhusu ujasiri wa Mgombea Urais kupitia CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan, ulivyoliwezesha Taifa kuvuka katika kipindi kigumu alipoingia madarakani.

Dk. Bashiru ambaye pia ni Mratibu wa Kampeni za Mgombea Urais Kanda ya Kati, alisema Dk. Samia kwa ujasiri, alifanikiwa kuivusha nchi salama baada ya kifo cha aliyekuwa Rais Dk. John Magufuli na mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO -19.

Akizungumza na maelfu ya wananchi waliofurika katika mkutano wa kampeni, uliofanyika Uwanja wa Bombadia, Singida Mjini, alisema hizo ni sababu za kutosha kumpa Dk. Samia, nafasi nyingine ya kuliongoza Taifa.

Katibu mkuu huyo mstaafu wa CCM, alisema alishiriki moja kwa moja katika vikao vya maamuzi ndani ya Chama ni shahidi namna Dk. Samia alivyoivusha nchi.

“Mnanijua mimi siyo mtu wa kupindisha. Hali haikuwa rahisi. Tulimpoteza kiongozi jasiri na wakati huo, tukakumbwa na COVID-19. Lakini, tulivuka salama. Huu ni ushahidi wa ujasiri wake.

“Nilikaa kimya kwa muda, lakini leo (jana), nimeibuka kwa nguvu mpya. Ushuhuda wangu ni wa wazi, Rais Samia ni kiongozi wa mfano.

“Msiwe na mashaka, ameshika nchi wakati mgumu na akatuvusha. Hiyo ni sifa tosha ya kuongezewa muda,”alibainisha.

Aliongeza kuwa, katika mazingira hayo, mataifa mengi huvurugika, ila Tanzania ilibaki yenye mshikamano kwa sababu ya utulivu wa Rais Dk. Samia na misingi imara ya Chama.

Dk. Bashiru, alisema uzoefu wake, unamtosha kusema wazi kwamba, Dk. Samia, ameonesha uongozi wa kiwango cha juu hasa katika usawa wa kijinsia na heshima ya binadamu.

“Usawa wa binadamu haumaanishi wote tuwe na kimo au rangi moja. Usawa ni kuheshimu utu wa kila mtu. Tajiri na maskini wakikosa maji au afya, wote wanadhalilika. 

“Ndiyo maana CCM inajenga shule, zahanati na kusambaza maji kulinda utu wa kila Mtanzania,” alisema.

Dk. Bashiru, alisema kwa muda mrefu, nafasi ya mwanamke imekuwa ya pili, kupitia uongozi wa Rais Dk. Samia, hali imebadilika na wanawake sasa wanaongoza mikoa, wilaya na majimbo kwa mafanikio makubwa.

“Nilikuwa nazungumza na Mwenyekiti wa Mkoa (Martha Mlatha). Singida mna RC (Mkuu wa Mkoa) mwanamke, RAS (Katibu Tawala Mkoa) mwanamke, Mwenyekiti wa CCM ni mwanamke na hakuna kilichoharibika.

Hii ni dalili ya kuaminika kwa wanawake,” alieleza.

Alisema hata katika majimbo ya uchaguzi, wanawake wamepewa nafasi na wanaendelea kuthibitisha uwezo wao wa kiuongozi bila doa.

Alisisitiza kuwa, misingi ya usawa, mshikamano na amani, ndiyo msingi wa umoja wa kitaifa na kwamba, serikali ya CCM, chini ya Dk. Samia, imeendelea kuilinda misingi hiyo.

Previous Post

JK AMWOMBEA KURA DK. SAMIA

Next Post

‘MIFUMO YA UUZAJI MAZAO YA WAKULIMA, WAIMARISHWA’

Next Post
‘MIFUMO YA UUZAJI MAZAO YA WAKULIMA, WAIMARISHWA’

‘MIFUMO YA UUZAJI MAZAO YA WAKULIMA, WAIMARISHWA’

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

3 months ago
MAAGIZO YA DK. MIGIRO KWA SHULE YA UONGOZI MWALIMU NYERERE

MAAGIZO YA DK. MIGIRO KWA SHULE YA UONGOZI MWALIMU NYERERE

3 months ago

Popular News

  • WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KILIO CHA BANDO CHATUA BUNGENI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ZIARA YA KIHONGOSI YAACHA NEEMA KWA WANAWAKE MARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YAJIPANGA KUDHIBITI MIJI HOLELA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?