• ePaper
Wednesday, June 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home AFYA

WASOMI, WANASIASA WAKOSHWA TOZO KUCHANGIA BIMA YA AFYA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
June 15, 2026
in AFYA, Habari, Kitaifa
0
WASOMI, WANASIASA WAKOSHWA TOZO KUCHANGIA BIMA YA AFYA
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na REHEMA MAIGALA

WASOMI na mwanasiasa, wameelezea manufaa ya mkakati wa serikali kutoza sh. 10 kila kilo moja ya sukari kwa lengo la kuwasilishwa katika Mfuko wa Bima ya Afya, wananchi wengi wapate huduma hiyo kwa urahisi.

Wamesema mbinu hiyo, itasaidia Watanzania wengi kupata huduma nzuri na kwa gharama nafuu.

Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, Alhamisi Juni 11, 2026, alitangaza hatua mpya za kimkakati kupunguza matumizi ya fedha taslimu, kuanzia Mwaka wa Fedha 2026/2027, zikiwa ni jitihada za kuimarisha uchumi wa kidijitali na kuongeza uwazi katika miamala ya fedha.

Balozi Omar alitangaza hatua hiyo alipowasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, jana, wanasiasa na wasomi hao, waliipongeza serikali kwa mkakati huo ambao utakuwa msaada mkubwa kwa Watanzania katika suala zima la afya.

DK. PHILIP DANINGA

Mhadhiri Mwandamizi wa Uchumi na Uongozi wa Chuo Cha Mwalimu Nyerere, Dk. Philip Daninga, aliunga mkono hatua ya serikali ya kutaka kukusanya sh. Bilioni 7.5 kupitia vyanzo vipya vya mapato vitakavyowezesha kugharamia utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.

Dk. Daninga, alisema huduma ya bima ya afya ni kitu muhimu kwa afya ya binadamu, ambayo itamwezesha mtumiaji kutumia fedha kidogo na kupata huduma kwa gharama nzuri na salama kwa afya yake.

Alisema serikali imeamua kubuni mkakati huo kwa upande wa bima ya afya, lengo ni kutaka kuwasaidia wananchi katika upande wa sekta ya afya baada ya gharama za huduma za matibabu kuwa juu.

“Mpango huu utakuwa mkombozi kwa Watanzania wengi, kwa sababu hadi leo hii, wapo baadhi ya watu wanapata maradhi, wanashindwa kwenda hospitali kwa kutokidhi gharama za matibabu.

Hivyo, kama kila mwananchi atakuwa na kadi yake ya bima ya afya, itarahisisha watu kupata huduma nzuri na bei nafuu,” alisema.

Dk. Daninga, alisema mtaji mkubwa wa binadamu ni afya njema, ambayo itamsaidia kufanya shughuli zake za uzalishaji mali.

DK. SYLVESTER RUGEIHYAM

Mtaalamu wa Somo la Hisabati na Mchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sylvester Rugeihyam, aliipongeza serikali kwa mkakati mzuri wa kuwapatia wananchi huduma ya afya.

Dk. Rugeihyam, alisema kupitia tozo ya sh. 10 kwa kila kilo moja ya sukari, serikali imerahisisha na lengo lake ni kutaka kila mwananchi apate huduma ya bima ya afya. tofauti na ilivyo hivi sasa.

“Ubunifu huu, utawasaidia wananchi wengi wakiwemo wa kipato cha chini na kati,  wote hao watapata huduma bora ya bima ya afya,”alisema.

HASSAN DOYO

Katibu Mkuu wa Chama cha NLD, Hassan Doyo, alisema ubunifu mpya katika vyanzo vya mapato ni miongoni mwa maendeleo nchini.

“Naipongeza serikali kwa ubunifu huo ambao utawarahisishia wananchi wengi kupata huduma ya afya,”alisema.

Doyo alipendekeza kuwa, huduma hiyo ya bima ya afya iendelee kudumu ni vyema serikali ingetoza sh. 100 kwa kila kilo 100 ya mahindi.

“Ubunifu huu wananchi wameufurahia tangu wausikie tunachoomba tunataka ufanikiwe na kila Mtanzania afaidie na mfuko wa Bima ya Afya kwa Wote,”alisema.

PILI MSELU

Mkazi Kinondoni Dar es Salaam, Pili Mselu, alisema  mikakati inayofanywa na serikali ya kutaka kila Mtanzania awe na bima ya afya imekuwa ni mkombozi kwake na watanzania wengine.

Mwishoni mwa wiki, Waziri wa Fedha, Balozi Khamisi Omar, alisema serikali inatarajia kukusanya sh. bilioni 7.5 kupitia vyanzo vipya vya mapato.

Balozi Omar alisema hayo bungeni, alipotangaza mkakati huo alipowasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.

Alisema hatua hiyo inatokana na mapendekezo ya sheria na kanuni yanayolenga kuongeza uwezo wa kifedha wa serikali katika sekta ya afya.

Previous Post

MWIGULU ASISITIZA UHURU WA KUABUDU

Next Post

MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

Next Post
MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MAJIJI SITA MOROCCO KUIPAMBA AFCON

MAJIJI SITA MOROCCO KUIPAMBA AFCON

6 months ago
MAMBO YAANZA KUNOGA MEI MOSI

MAMBO YAANZA KUNOGA MEI MOSI

2 months ago

Popular News

  • WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    WABUNGE WAIPONGEZA NSSF NA PSSSF KWA KUANZISHA SKIMU YA HIFADHI KWA WALIOJIAJIRI NA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA NGOZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WABUNGE WAPONGEZA UWEKEZAJI KLICL

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAKAGUZI WA CAF WARIDHISHWA NA MAENDELEO YA VIWANJA VYA AFCON 2027

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MKAKATI KUDHIBITI VIFO WAJAWAZITO WAANIKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WASOMI, WANASIASA WAKOSHWA TOZO KUCHANGIA BIMA YA AFYA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?