• ePaper
Thursday, July 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

ALIYEOA MWANAFUNZI KWA MAHARI MILIONI 4/- ADAKWA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
July 30, 2026
in Habari, Kitaifa
0
ALIYEOA MWANAFUNZI KWA MAHARI MILIONI 4/- ADAKWA
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

SALVATORY NTANDU, Shinyanga

MKAZI wa Kijiji cha Lyabukande, Bundala Mashiku, amekamatwa kwa tuhuma za kuoa mwanafunzi wa kidato cha tano kwa ahadi ya mahari ya sh. milioni 4.5.

Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Julias Mtatiro, ilimkamata Bundala (24), ambaye alitarajia kulipa mahari hiyo Agosti 5, mwaka huu.

Akizungumza katika msako huo, Mtatiro alisema mwanafunzi huyo alichaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika Shule ya Sekondari Kili iliyopo wilayani Nzega Mkoa wa Tabora, ambapo wazazi wake walimwozesha kwa familia ya Mashiku Sylivesta.

Alisema serikali haitavumilia kuona uozeshaji wanafunzi ukiendelea, hivyo Bundala, baba yake Mashiku, watashikiliwa na vyombo vya usalama na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

“Natangaza vita kwa wazazi ambao wameozesha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu, tunaendelea na msako wa kila familia ili kuhakikisha wote waliochaguliwa wanaenda shule kutimiza ndoto zao,”alisema Mtatiro.

Aidha, Mtatiro aliwataka wazazi kuacha tamaa ya mali kuozesha wanafunzi kwa kuwa sheria zipo na zinaendelea kufanya kazi.

“Watakaobainika watakamatwa na kufikishwa mahakamani kitendo hiki hakifai kuigwa katika jamii na kila mwananchi anapaswa kukikemea,” alisema Mtatiro.

Kwa upande wake, Mashiku alidai hakujua kama binti huyo  ni mwanafunzi na alikubaliana kulipa mahari ya sh. milioni tatu Agosti 5 na mwakani angemalizia sh. milioni 1.5, baada ya kuishi nyumbani kwake miezi miwili.

“Kijana wangu alichumbia mke akamleta nyumbani, familia tukakubaliana kulipa mahari. Sikujua kama ni mwanafunzi nilifahamu alimaliza kidato cha nne mwaka jana sikuwa na wasiwasi,”alisema.

Awali, Bundala alidai hakuwa akifahamu kama mke wake ni mwanafunzi aliyefaulu kujiunga na kidato cha tano.

Previous Post

AGGREY MWANRI NAIBU KATIBU MKUU CCM

Next Post

SERIKALI KUANGALIA FURSA ZA MIKOPO KWA WANAOSOMA KOZI FUPI – WAZIRI MKUU

Next Post
SERIKALI KUANGALIA FURSA ZA MIKOPO KWA WANAOSOMA KOZI FUPI – WAZIRI MKUU

SERIKALI KUANGALIA FURSA ZA MIKOPO KWA WANAOSOMA KOZI FUPI - WAZIRI MKUU

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CHANETA IMANI KIBAO NA TUME HURU YA UCHUNGUZI

CHANETA IMANI KIBAO NA TUME HURU YA UCHUNGUZI

4 months ago
YANGA, AZAM FC FAINALI YA KIBABE

YANGA, AZAM FC FAINALI YA KIBABE

7 months ago

Popular News

  • SERIKALI KUZALISHA MAELFU YA AJIRA KWA VIJANA KUPITIA MRADI WA UCHIMBAJI WA VISIMA VYA UMWAGILIAJI

    SERIKALI KUZALISHA MAELFU YA AJIRA KWA VIJANA KUPITIA MRADI WA UCHIMBAJI WA VISIMA VYA UMWAGILIAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • PPAA YAHIMIZA WAZABUNI KUTUMIA MODULI YA MALALAMIKO NA RUFAA KATIKA MFUMO WA NeST

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI KUANGALIA FURSA ZA MIKOPO KWA WANAOSOMA KOZI FUPI – WAZIRI MKUU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ALIYEOA MWANAFUNZI KWA MAHARI MILIONI 4/- ADAKWA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • AGGREY MWANRI NAIBU KATIBU MKUU CCM

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?