• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 6, 2025
in Habari, Kitaifa
0
CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI CHAMPONGEZA JOHARI
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

CHAMA cha Mawakili wa Serikali (GAT) kimempongeza, Hamza Johari kwa kuteuliwa tena kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kikiuelezea uteuzi huo kuwa ni kielelezo cha ubobezi na uadilifu wake katika taaluma ya sheria.

Kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho, uteuzi huo pia unaendana na matakwa ya Ibara ya 59 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayotaka Mwanasheria Mkuu awe na sifa za uwakili kwa angalau miaka 15.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Johari ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika utumishi wa umma, hususan katika masuala ya mikataba, sheria za anga, bahari na udhibiti.

Ana Shahada ya Sheria (LL.B) na Shahada ya Uzamili (LL.M) katika Sheria za Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Kiev, Ukraine, pamoja na cheti cha Uongozi na Usimamizi kutoka Chuo cha Utawala cha India.

Johari amewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kwa kipindi cha miaka tisa, na pia amehudumu kama Mwenyekiti wa CANSO Afrika, CASSOA na kamati mbalimbali za kisheria za kikanda na kimataifa.

Aidha, amewahi kufundisha katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu cha Alexandria nchini Misri.

Mbali na hayo, Johari amekuwa Mlezi wa Chama cha Mawakili wa Serikali, Mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, na Mwenyekiti wa timu za majadiliano ya Serikali katika mikataba mikubwa ya kimataifa ikiwemo ya DP World (U.A.E) na Bandari ya Adani (India).

Pia ameshiriki katika timu za kitaifa za kutatua migogoro ya mipaka na majadiliano ya miradi ya kimkakati ya kitaifa.

Johari ni Mmakonde, mzaliwa wa Wilaya ya Mtwara Vijijini, Tarafa ya Ziwani, Kata ya Nalingu.

Previous Post

WATALII WAENDELEA KUFURIKA NGORONGORO, WASIFU AMANI NA VIVUTIO VYA TANZANIA

Next Post

GAMONDI AMPA MAJUKUMU KELVIN JOHN

Next Post
GAMONDI AMPA MAJUKUMU KELVIN JOHN

GAMONDI AMPA MAJUKUMU KELVIN JOHN

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

YANGA, SIMBA KAZI KAZI

5 months ago
RAIS DK. SAMIA AMPA   ZAHIR ZORRO MILIONI 10/-

RAIS DK. SAMIA AMPA   ZAHIR ZORRO MILIONI 10/-

1 month ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?