• ePaper
Sunday, June 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TUME YAUNDWA KUBAINI TUHUMA UZIMAJI X -RAY

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 30, 2025
in Habari, Kitaifa
0
TUME YAUNDWA KUBAINI TUHUMA UZIMAJI X -RAY
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ATHNATH MKIRAMWENI

SERIKALI imeunda tume maalumu kuchunguza tuhuma za utendaji usioridhisha zinazoikabili Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke.

Kazi nyingine itakayofanywa na tume hiyo ni tuhuma za kuzimwa mashine za X-Ray.

Kauli hiyo, ilitolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dk. Seif Shekalaghe, siku chache baada ya Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa kufanya ziara katika hospitali hiyo na kubaini changamoto kadhaa.

“Tumeandaa kamati maalumu ya kuchunguza tuhuma hizo na inaendelea na kazi yake, watakapokamilisha uchunguzi tutatoa taarifa, kwa maana kitu kinachofanyika kwa sasa ni uchunguzi wa kina wa tuhuma hizo,” alisema.

Hivi karibuni, serikali ilitangaza kuanza msako mkali dhidi ya watumishi wa afya wanaodaiwa kuhujumu utoaji huduma kwa makusudi na kusababishwa wagonjwa kukosa huduma ndani ya hospitali za umma na kulazimika kwenda binafsi.

Kauli hiyo, ilitolewa hivi karibuni na Mchengerwa, kuwepo tuhuma za kuzimwa mashine za X-ray katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke.

Kitendo hicho, kilisababisha wagonjwa kukosa huduma muhimu na kuelekezwa kwenda katika zahanati na maeneo mengine binafsi kupata matibabu.

Alisema watumishi wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo, watachukuliwa hatua kali za kisheria bila muhali.

Alisisitiza kuwa, serikali haitavumilia hujuma zinazolenga kunufaisha sekta binafsi kwa kuwaumiza wananchi.

Mchengerwa, alisema uchunguzi wa awali, umedai kuwa, baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu, walizima mashine za X-ray kwa makusudi, licha ya kuwa vifaa hivyo vinafanya kazi.

Alisema taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuhusu kuwepo kwa mashine za X-ray zisizofanya kazi katika Hospitali ya Temeke, hazina ukweli wowote, isipokuwa ni matokeo ya hujuma zilizopangwa.

“Mashine zote za X-ray zilizopo Temeke, zinafanya kazi na zimesimikwa kupitia uwekezaji mkubwa wa Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha huduma za afya nchi nzima,” alisema.

Alisema baada ya kupokea taarifa hizo, aliagiza kufanyika uchunguzi wa kina kubaini ukweli wake.

Uchunguzi uliofanyika, ulibaini kuwa hujuma hizo, zilisababisha wagonjwa kukosa huduma ndani ya hospitali na kulazimika kupata huduma katika vituo binafsi.

Mchengerwa, alieleza vitendo hivyo ni usaliti mkubwa kwa serikali na wananchi kwamba, uchunguzi unaendelea kuwabaini wahusika wote.

“Natoa onyo kali kwa watumishi wote wa sekta ya afya, yeyote atakayehujumu huduma za afya kwa makusudi atachukuliwa hatua kali za kisheria na kinidhamu, zikiwemo kufukuzwa kazi na kutopata ajira yoyote ndani ya hospitali na kama ni daktari, tutamnyang’anya cheti chake na hatafanya kazi hata nje ya Tanzania,” alisisitiza.

Mchengerwa aliwahakikishia wananchi kuwa, serikali itaendelea kusimamia kwa ukaribu utoaji wa huduma za afya na kuhakikisha vifaa vyote vinavyonunuliwa kwa fedha za umma vinatumika ipasavyo kwa manufaa ya wananchi.

Previous Post

MSIGWA AELEZA MANUFAA UBORESHAJI RELI YA TAZARA

Next Post

SIKU YA HISTORIA MPYA TAIFA STARS

Next Post
SIKU YA HISTORIA MPYA TAIFA STARS

SIKU YA HISTORIA MPYA TAIFA STARS

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. GWAJIMA AONYA ‘WATU WAZIMA OVYO’ MITANDAONI

DK. GWAJIMA AONYA ‘WATU WAZIMA OVYO’ MITANDAONI

6 months ago
HALI YA USALAMA MKOA WA ARUSHA NI SHWARI – RC MAKALLA

HALI YA USALAMA MKOA WA ARUSHA NI SHWARI – RC MAKALLA

7 months ago

Popular News

  • RAIS DK. SAMIA ATAKA MIKOPO ISIWE MZIGO

    RAIS DK. SAMIA ATAKA MIKOPO ISIWE MZIGO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • AFRIKA KUCHOCHEA UTUNZAJI MAZINGIRA KUPITIA NISHATI SAFI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWAKINYO AOMBA RADHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • YANGA, SIMBA NI KIVINGINE ZAIDI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MEXICO YAANZA KWA KISHINDO WC, KADI ZATEMBEA HATARI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?