• ePaper
Saturday, May 2, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Makala

WATOTO HAWASTAHILI KUCHOMWA VIGANJA KWA KUDOKOA NYAMA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
January 17, 2026
in Makala
0
WATOTO HAWASTAHILI KUCHOMWA VIGANJA KWA KUDOKOA NYAMA
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na Mwandishi Wetu

KUMEKUWA na matukio ya ukatilki dhidi ya watoto kwa kiwango cha mtu kujiuliza kulikoni!

Serikali imekuwa ikichukua hatua dhidi ya uhalifu huo na mahakama imetoa adhabu kwa watenda ukatili, lakini hali haijakoma.

Ukatili dhidi ya watoto ambao hawawezi kujitetea kwa hili ama lile, umeendelea kutendwa na watu ‘makatili’ kwa viwango vya kutisha.

Watoto hufanyiwa ukatili wa aina mbalimbali; wa kijinsia, kimwili, kihisia, kisaikolojia na ule wa kingono ukijumuisha ubakaji na ulawiti.

Mama anashikwa na hasira inayoitwa ‘hasira kali’, anachukua mfuko wa ‘rambo’ anaufunga katika mikono ya mtoto na kuutia motoni.

Mikono ya mtoto inaungua; akiulizwa kisa cha yote hayo anajibu kadokoa mboga ya kuliwa jioni; hivi ni mtu mzima gani ambaye katika maisha ya utotoni hakuwahi kudokoa mboga?

Kama kuna watu wazima ambao hawajapitia utundu huo, hawawezi kujaa kiganjani, ni wachache na si ajabu anayemuadhibu mtoto kwa kiwango cha kumsababishia ulemavu wa maisha, alikuwa ni mdokozi ‘nambari wani’, lakini mama yake hakumtia motoni.

Watoto nyumbani kudokoa kitoweo au vyakula vingine ni sehemu ya makuzi yao; kinachotakiwa ni mzazi au mlezi kumkanya kwa adhabu isiyo ya kikatili, lakini itakayompa fundisho kwamba kudokoa dokoa ni tabia mbaya.

Udokozi wa sukari na maziwa ya unga unapendwa na watoto, hata wazazi wakiwakamata na kuuliza nani kadokoa sukari au maziwa, hakuna anayesema.

Sukari na maziwa ya unga, huwaumbua watoto wengi kwa sababu ushahidi ubaki nje ya mdomo, chembechembe za sukari au maziwa mama anapoziona, huuliza kuona watoto ni wa kweli kiasi gani, lakini mdokozi atakataa kuwa mdokozi ni yeye.

Iwapo kila mzazi angechoma moto mikono ya watoto wadokozi wa kitoweo; hasa nyama; nchi hii ingekuwa na watu katika makovu wengi sana wakiwemo viongozi wanaoheshimika.

Utoto ni hatua ya makuzi ya aina yake, weka maziwa ‘freshi’ kwenye friji kama hutakuta yameongezwa maji, unadhani nini kimefanyika? Je, utamchoma mdomo au ulimi?

Weka kopo la maziwa ya ‘laktojeni’ kwa ajili ya mdogo wao anayenyonya, kama hutakuta yamepungua kwa kiwango cha kutisha.

Utawaita kuwauliza nani amebugia maziwa ya mtoto, jibu litakuwa “siyo mimi mama”, tosheka na jibu hilo, toa adhabu za ‘saizi’ yao tena kwa busara siyo kuchoma moto viungo vya watoto, majuto ni mjukuu.

Watoto wanakimbia nyumbani wanatupa nguo za shule na mikoba ya madaftari porini, hawataki kurudi nyumbani kutokana na ukatili wanaofanyiwa, wanaona heri kulala nje mitaani!

Mtoto amekosa kakosa kidogo tu, mama wa kambo anamchongea kwa baba ambaye akili zake nazo ‘zimetekwa’ kimapenzi, anamuadhibu kikatili mtoto wake kwa ajili ya ‘kumfurahisha mamsapu’.

Nini kinachotakiwa kufanyika ili kukabiliana na ukatili ambao unafanyika dhidi ya watoto kwa sababu mbalimbali na kwa viwango tofauti nyenye madhara anuai hadi wengine kusababishiwa vifo, vilema vya maisha na hata kupotelea mitaani?

Kunahitajika busara katika kuwaadhibu watoto na siyo hasira, hasa ikizingatiwa ukatili wa aina mbalimbali una madhara makubwa kwa watoto; kiakili, kisaikolojia, kinafsi na kimwili.

Matukio ya watoto kwenda kinyume na inavyotarajiwa, yanaweza kusababisha uchungu na hasira, lakini kunahitaji busara siyo hasira za kuumiza watoto.

Ukatili dhidi ya watoto ni changamoto inayohitaji kushughulikiwa kwa haraka na kwa umakini. Ni jukumu la kila Mtanzania  kuhakikisha haki na ustawi wa watoto unalindwa.  

Ukatili kwa watoto husababisha athari kubwa na madhara ya muda mrefu. Watoto wanaokumbwa na ukatili wanaweza kupata sonona, wasiwasi, na msongo wa mawazo. 

Kuwa na majeraha na magonjwa yasiyopona, ukuaji na ustawi wao kudorora. Watoto walio na wanaofanyiwa ukatili hukosa kujiamini na huona ni bora kujitenga na jamii.

Kumekua na matukio ya kusikitisha na kukasirisha ya vitendo vya kinyama na kikatili dhidi ya watoto kwa sababu ya watu wazima kushindwa kuzuia hasira zao.

Imani za kishirikina nazo zinachangia ukatili kwa watoto kwa sababu imefikia hatua baba anambaka mtoto wake kutimiza masharti ya mganga wa kinyeji kwamba akifanya ukatili huo atatajirika.

Mtu mzima badala ya kufanya kazi kwa bidii ili kupata utajiri, anatekeleza ushauri wa kijinga wa kumfanyia ukatili mtoto wake wa kumzaa bila aibu!

Katika matukio mengine baba wamezaa na mabinti zao; hii ni fedheha na ukatili mkubwa kwa sababu hata mtoto azaliwaye akikua na kujitambua, atajisikia vibaya na kupata athari za aina mbalimbali kwa sababu ya kitendo cha mtu mzima mmoja hovyo.

Katika matukio mengine katika jamii za kiafrika watoto wametolewa kafara au kufanyiwa vitendo vya kikatili kama sehemu ya matambiko ya kimila yanayodhaniwa kuleta utajiri au kuondoa mikosi.

Ni jukumu la kila mtu mzima kupinga ukatili vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto. Kuna watu ambao wamekuwa ni mfano bora wa kuiga kwa kutoa taarifa na serikali kuingilia kati kunusuru watoto.

 Adhabu kali zinapaswa kutolewa kwa wale wanaopatikana na hatia ya ukatili dhidi ya watoto. Ni muhimu kuwa na utekelezaji madhubuti wa sheria kuhakikisha wale wanawafanyia watoto ukatili wanachukuliwa hatua kali za kisheria.

Vyombo vya habari rasmi na visivyo rasmi, vinapaswa ‘kupaza’ sauti pale waandishi wake wa habari wanapoona kuna mtoto au watoto wanapitia kwenye ukatili.

Ni muhimu kuimarisha huduma za ushauri nasaha na matibabu kwa watoto waliokumbwa na ukatili kuwasaidia kupona na kurudi katika hali zao za kawaida.

 Ushirikiano kati ya serikali, jamii na wadau wengine wa masuala ya watoto, ni muhimu ukaimarishwa kwa kuwekeza rasilimali na utaalamu kupitia kampeni za kuondoa ukatili wa aina zote dhidi ya watoto.

Ni jukumu la wote kuhakikisha  watoto wanakua katika mazingira salama yanayowawezesha kustawi huku wakifurahia maisha ya kuwa watoto.

Previous Post

WATALAMU WATAJA KINGA ZA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

Next Post

DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

Next Post
DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

DK. SAMIA AMREJESHA MAKONDA AFCON

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TANZANIA YAJIPANGA KUNUFAIKA NA GESI TRILIONI 57.54, WAWEKEZAJI WAALIKWA

TANZANIA YAJIPANGA KUNUFAIKA NA GESI TRILIONI 57.54, WAWEKEZAJI WAALIKWA

1 month ago
DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

DK. SAMIA AAHIDI UCHUMI JUMUISHI

7 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?