MENEJA wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema huo ni mchezo wa jasho na damu kwani wanahitaji kupata ushindi ili kujiweka salama.
“Tunakwenda kupambana kwa ajili ya kupata pointi tatu muhimu, lengo letu ni kuhakikisha tunatinga robo fainali ya mashindano hayo,”alisema.
Ahmed alisema wamepoteza mechi zote mbili katika kundi lao, lakini hawatakubali kupoteza mchezo huo na mingine iliyobaki.
Ofisa habari wa Yanga, Ali Kamwe alisema wanahitaji zaidi miguu ya wachezaji ifanye kazi kuliko maneno.
Kamwe alisema yanaweza kuzungumzwa maneno mengi, lakini ukweli muda umefika hawahitaji maneno zaidi ya wachezaji wao kuonesha kwa vitendo kwa kupambana uwanjani kutafuta ushindi.
“Wachezaji wanatambua nini wanatakiwa kukifanya, nimepata bahati ya kuzungumza nao wamesema wanajua jukumu walilonalo na namna gani wanachama na mashabiki wanawategemea. Mimi naweza kuzungumza maneno mengi, lakini ukweli tunahitaji miguu ya wachezaji zaidi na si maneno,” alisema Kamwe.
USO KWA USO
Wachezaji wa Yanga na Simba walikutana jana, alfajiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, kila mmoja akiwa anaelekea katika majukumu ya mechi ya mashindano ya kimataifa ya Shirikisho la Soka Afrika(CAF).




