• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA ATAJA FAIDA ZA MPANGO WA NISHATI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 15, 2026
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA ATAJA FAIDA ZA MPANGO WA NISHATI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ametaja faida za Mpango wa Nishati wa Tanzania, akisema utaongeza upatikanaji wa nishati safi na kuimarisha mageuzi ya kiuchumi.

Aidha, amebainisha mpango wa taifa wa kuwekeza katika vyanzo vya nishati jadidifu, ikiwemo ya jua, upepo, jotoardhi, umeme wa maji endelevu na kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Rais Dk. Samia alieleza hayo, jijini Addis Ababa, Ethiopia, aliposhiriki Mkutano wa Kamati ya Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika wanaosimamia Mabadiliko ya Tabianchi (CAHOSCC), pembezoni mwa Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika.

MABADILIKO YA TABIANCHI

Akizungumza katika mkutano huo, Rais Dk. Samia alieleza kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuathiri kwa kiasi kikubwa sekta muhimu za uchumi na zinazozalisha ajira, ikiwemo ya kilimo, nishati, uvuvi, utalii na miundombinu.

Dk. Samia alisema hali ya hewa isiyotabirika inaendelea kudhoofisha mifumo ya maisha na uzalishaji barani Afrika.

Rais Samia alisema, ndiyo maana Tanzania inatekeleza mkakati huo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, unaolenga kupanua upatikanaji wa nishati safi na kuimarisha mageuzi ya kiuchumi.

Alibainisha mpango huo wa taifa wa kuwekeza katika vyanzo vya nishati jadidifu, ikiwemo jua, upepo, jotoardhi, umeme wa maji endelevu na kuimarisha matumizi ya nishati safi ya kupikia una tija kubwa katika kukabili mabadiliko hayo ya tabianchi.

Vilevile, Rais Dk. Samia alitaja ajenda ya nishati safi ya kupikia kuwa, kipaumbele cha taifa kinacholingana na mwelekeo wa Afrika katika mabadiliko ya sekta ya nishati.

USHIRIKIANO WA KIKANDA

Kwa mujibu wa Rais Samia, kupitia miundombinu ya pamoja ya kikanda, Tanzania inaendelea kuchangia usalama wa nishati na mshikamano wa kiuchumi barani Afrika, hatua inayoongeza uwezo wa nchi kukidhi mahitaji ya uzalishaji, huduma za kijamii na ukuaji wa viwanda.

Rais Dk. Samia alisisitiza umuhimu wa kuimarisha mifumo ya utabiri na usimamizi wa majanga kwa kushirikiana na taasisi za kikanda, kwa lengo la kuchukua tahadhari za mapema.

“Taarifa za hali ya hewa kwa wakati huokoa maisha na kupunguza gharama za kukabiliana na majanga,”alisema Rais.

CHANGAMOTO

Hata hivyo, alibainisha tatizo la mifumo hiyo kukabiliwa na changamoto za upungufu wa rasilimali, hivyo kuhitaji kupewa kipaumbele katika ushirikiano wa kimataifa.

Rais aliongeza kuwa, mfumo wa kimataifa wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi unategemea utekelezaji wa ahadi za kifedha kwa wakati na kwa ufanisi.

Alitaja utaratibu mgumu, gharama kubwa za utekelezaji na utegemezi mkubwa wa mikopo ni kikwazo endelevu kwa nchi zenye uwezo mdogo wa kifedha, huku akisisitiza umuhimu wa ruzuku na masharti nafuu ya fedha katika kulinda mafanikio ya maendeleo.

“Kwa Tanzania na nchi nyingi za Afrika, ufadhili wa ruzuku kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na fedha za masharti nafuu ni muhimu katika kulinda mafanikio ya maendeleo, huku zikikabiliana na hatari za mabadiliko ya tabianchi,”alisisitiza.

MALENGO YA DUNIA

Halikadhalika, alisema Tanzania inaunga mkono Malengo ya Dunia ya Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi na inaendelea kushirikiana kwa karibu na Kituo cha Afrika cha Matumizi ya Takwimu na Taarifa za Hali ya Hewa kwa Maendeleo (ACMAD) na taasisi za kikanda, kuimarisha mifumo ya tahadhari za mapema.

Alitumia kikao hicho kusisitiza kuwa, mifumo hiyo inahitaji kuimarishwa zaidi kifedha na kutambuliwa kama rasilimali ya pamoja ya kimataifa.

Pia, Rais Dk. Samia aliunga mkono juhudi za kuanzisha viwango vya pamoja vya Afrika katika masoko ya kaboni, akieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu kuhakikisha biashara hiyo inaleta manufaa halisi kwa jamii, taifa na kulinda mazingira.

Rais Samia alibainisha hatua zinazochukuliwa na Tanzania kuongeza thamani ya rasilimali, madini ya kijani, utalii endelevu, na miundombinu inayostahimili mabadiliko ya tabianchi, kama sehemu ya kujenga uchumi jumuishi na unaozalisha ajira.

Dk. Samia alisema Tanzania ipo tayari kushirikiana kwa karibu na nchi nyingine za Afrika, katika maandalizi ya mikutano ijayo ya kimataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi, kuhakikisha vipaumbele vya bara hilo vinapata msukumo wa kisera na kiutendaji.

Alisema kuwa mafanikio ya pamoja yatategemea uratibu madhubuti kati ya serikali, taasisi za kikanda na taasisi za bara.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AGEUKIA VITA DHIDI YA MALARIA 

Next Post

CHINA YAENDELEZA UHUSIANO, USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KWA BARA LA AFRIKA

Next Post
CHINA YAENDELEZA UHUSIANO, USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KWA BARA LA AFRIKA

CHINA YAENDELEZA UHUSIANO, USHIRIKIANO WA KIMKAKATI KWA BARA LA AFRIKA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

RAIS DK. SAMIA KUONGOZA SHUGHULI YA KUMUAGA LUKUVI DAR

RAIS DK. SAMIA KUONGOZA SHUGHULI YA KUMUAGA LUKUVI DAR

3 weeks ago
DK. MWIGULU ATAKA KASI USAMBAZAJI GESI ASILIA

DK. MWIGULU ATAKA KASI USAMBAZAJI GESI ASILIA

2 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?