• ePaper
Wednesday, April 15, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

DK. NCHIMBI : KUMBUKIZI ZA MAJIMAJI ZIWE CHACHU YA UZALENDO NA UWAJIBIKAJI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
February 27, 2026
in Habari, Kitaifa
0
DK. NCHIMBI : KUMBUKIZI ZA MAJIMAJI ZIWE CHACHU YA UZALENDO NA UWAJIBIKAJI
0
SHARES
9
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi, amesema Mashujaa wa Vita ya Majimaji wanapaswa kuenziwa kwa kuimarisha nidhamu katika utendaji kazi, kupinga ukabila na kutambua wajibu wa kila Mtanzania katika kulitetea na kulijenga Taifa.

Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa kilele cha Tamasha la 17 la Kumbukizi ya Miaka 120 ya Mashujaa wa Vita ya Majimaji, lililofanyika katika Viwanja vya Makumbusho ya Vita ya Majimaji, Songea, mkoani Ruvuma.

Amesema ni muhimu kuenzi mchango wa mashujaa hao kwa kuendelea kusimamia umoja wa kitaifa, kuhakikisha makabila yote yanaishi kama Taifa moja, kufanya kazi kwa bidii katika kuijenga nchi, pamoja na kupinga vitendo vya rushwa na kusimamia haki.

Ameongeza kuwa mashujaa wa Vita ya Majimaji waliweka pembeni ubinafsi kwa kuunganisha zaidi ya makabila 30 kupambana na wakoloni, jambo lililoweka msingi wa mustakabali bora wa Taifa la leo.

Makamu wa Rais amesema kumbukizi za Vita ya Majimaji ni nyenzo muhimu kwa kizazi cha sasa na kijacho kujifunza uzalendo, ujasiri na kujitolea, kwani mashujaa hao walitoa maisha yao kulinda heshima, utu na rasilimali za Taifa.

Aidha, ametoa wito kwa jamii kushirikiana na Shirika la Makumbusho ya Taifa kuanzisha makumbusho katika maeneo yao kwa lengo la kuhifadhi historia ya Taifa na kutumia fursa zilizopo katika malikale kukuza uchumi kupitia utalii wa utamaduni.

Amesema maboresho yaliyofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii katika Sheria ya Malikale, Sura ya 333 na Sheria ya Makumbusho ya Taifa, Sura ya 281, yamefungua fursa kwa jamii na taasisi binafsi kuanzisha makumbusho.

Vilevile, Makamu wa Rais amezihimiza taasisi binafsi na jamii kwa ujumla kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kuwekeza katika kumbukumbu na malikale zilizopo nchini, kama chanzo cha ajira, pamoja na majukwaa ya kutangaza bidhaa, vivutio vya uwekezaji na utalii.

Previous Post

MOTO WA DK. MWIGULU HAUPOI

Next Post

MWISHO WA ENZI

Next Post
MWISHO WA ENZI

MWISHO WA ENZI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CHAMBUA: DUBE KAMA MAYELE

CHAMBUA: DUBE KAMA MAYELE

4 months ago
TANZANIA TUNA RAIS JASIRI NA MCHAPAKAZI

TANZANIA TUNA RAIS JASIRI NA MCHAPAKAZI

3 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?