• ePaper
Sunday, May 31, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

NAIBU WAZIRI MAGHEMBE AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA DHARURA WA SADC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
December 17, 2025
in Habari, Kitaifa
0
NAIBU WAZIRI MAGHEMBE AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA DHARURA WA SADC
0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUM

NAIBU Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ngwaru Maghembe, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kilichofanyia leo Desemba 17, 2025.

Dk. Maghembe ameshiriki kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) katika kikao hicho kilichofanyika kwa njia ya mtandao.

Kikao hicho kimefunguliwa na kuongozwa na Waziri wa Mahusiano ya Kimataifa na Ushirikiano wa Jamhuri ya Afrika Kusini na Mwenyekiti wa Mpito wa Baraza la Mawaziri, Ronald Lamola, ambapo nchi wanachama zimejadili hali ya kisiasa na usalama katika Jamhuri ya Madagascar.

Aidha, Kikao kimepokea na kuridhia pendekezo la Jamhuri ya Zambia kushika nafasi ya Mwenyekiti Ajaye wa Mpito kufuatia Jamhuri ya Afrika Kusini kushika nafasi ya Mwenyekiti wa Mpito wa SADC.

Mawaziri hao pia wamepitisha bajeti kwa ajili ya kuiwezesha SADC kutekeleza jitihada zake za kuisaidia Madagascar kupata ufumbuzi wa changamoto zilizopo.

Mkutano huo wa mawaziri umetanguliwa na Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kilichofanyika asubuhi ya leo Desemba 17, 2025, ambapo Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Dk. Samwel Shelukindo aliongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho.

Balozi Shelukindo ameungana na wadau kutoka sekta mbalimbali nchini akiwemo Naibu Katibu Mkuu wizarani, Balozi Said Shaib Mussa, pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania, Lut. Jen. Salum Haji Othman.

Previous Post

SERIKALI MATUMAINI KIBAO AFCON

Next Post

MAGAMBO AAHIDI KUENDELEZA MAFANIKIO YA PSSSF

Next Post
MAGAMBO AAHIDI KUENDELEZA MAFANIKIO YA PSSSF

MAGAMBO AAHIDI KUENDELEZA MAFANIKIO YA PSSSF

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

MRADI WA UMEMEJUA KISHAPU KULETA MAPINDUZI SEKTA YA NISHATI – MAKAMBA

5 months ago
KOCHA SIMBA KICHEKO  

KOCHA SIMBA KICHEKO  

2 weeks ago

Popular News

  • SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    SERENGETI BOYS KILA KONA, RAIS SAMIA AWAPA MILIONI 500/-

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?