Na MWANDISHI WETU
HALI nzuri ya usalama imeifanya Tanzania kuwa kivutio na kituo muhimu kuwezesha Mkufano wa Mabunge Duniani (IPU). kufanyika nchini, hivyo kuleta fursa mbalimbali za kiuchumi na kibiashara ikiwemo sekta ya utalii.
Hatua hiyo inaonyesha zaidi ya wabunge 2000 wa IPU watatua nchini, kuhudhuria mkutano huo.
Tayari banda la maonesho la Tanzania limegeuka kuwa kivutio kikubwa na wageni wengi wanaohudhuria Maonyesho ya Utalii Uturuki, wamefika kushuhudia na kuelezwa kuhusu vivutio mbalimbali vya utalii na fursa zilizopo katika sekta hiyo nchini Tanzania.
HALI YA USALAMA
Kutokana na kuridhishwa na kufurahishwa kuhusu vivutio vya Tanzania na hali ya usalama mkubwa, wageni wengi waliofika katika Mkutano huo pia walijiandikisha kwa wingi na kuthibitisha kushiriki mkutano wa 153 wa IPU utakaofanyika mkoani Arusha, Oktoba, mwaka huu.
Katika mkutano huo utakaofanyika nchini, zaidi ya Wabunge 2000 wa Mabunge ya Dunia wakiongozwa na Maspika wa Mabunge yao Duniani, wanategemewa kuhudhuria mkutano huo.
Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii (TTB), Vivian Temu, amenukuliwa katika taarifa iliyopatikana jijijini Dares Salaam leo, akisema bodi hiyo imejipanga kuhakikisha wabunge hao wa IPU wanapata fursa kutembelea vivituo vya utalii nchini watakaposhiriki mkutano wao mwezi Oktoba.



