• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 6, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO
0
SHARES
1
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, ameizindua na kuipa maagizo matano Bodi ya Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) kilichopo mkoani Morogoro.

Ametoa maagizo hayo jijini Dar es Salaam Machi 6, 2026, ambapo ameelekeza bodi  kuimarisha mifumo ya kitaifa ya Upimaji, Utoaji Taarifa na Uhakiki wa gesijoto (MRV), kuhakikisha taarifa za kaboni nchini zinakuwa sahihi, za kuaminika na zinazokubalika kimataifa.

Pia, ameitaka kuhakikisha Miradi yote ya kaboni inayotekelezwa nchini inasimamiwa kwa ufanisi, uwazi na kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa pamoja na maslahi mapana ya taifa.

Waziri Masauni amesema bodi hiyo inapaswa kuweka mazingira wezeshi yatakayovutia uwekezaji wa ndani wa kimataifa katika sekta ya kaboni, huku ikihakikisha uwekezaji huo unalinda rasilimali za taifa na kuleta manufaa ya kweli kwa wananchi, kuhakikisha kunakuwepo mfumo wa haki na uwazi wa mgawanyiko wa manufaa, jamii zinazohifadhi rasilimali za asili zinufaike moja kwa moja na miradi ya Kaboni inayotekelezwa katika maeneo yao.

“Kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika mifumo ya kimataifa ya biashara ya kaboni hususan chini ya Ibara ya 6 ya Mkataba wa Paris, ikiwemo mifumo ya soko la kaboni kuongeza fursa za kiuchumi kwa taifa letu,” amesema Masauni.

Aidha, ameisisitiza bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha kituo kinaendeshwa kwa uwajibikaji, uadilifu na weledi wa hali ya juu kuhakikisha mifumo ya usimamizi wa sekta ya kaboni inalinda kikamilifu maslahi ya taifa.

“Ni matarajio ya serikali kuona kituo hiki kinakuwa kitovu cha ubora katika masuala ya ufuatiliaji wa kaboni, biadhara ya kaboni na tafiti za mabadiliko ya tabianchi katika ukanda wa Afrika. Haya ni matarajio makubwa kwa taifa letu na yanahitaji usimamizi madhubuti wa taasisi, mifumo imara ya ufuatiliaji pamoja na ushirikiano wa wadau wote,” alisema.

Aliongeza matarajio ya serikali yaliyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, na Mpango wa muda mrefu wa utekelezaji wake, sekta ya kaboni ina uwezo wa kuchangia takribani Dola za Marekani bilioni mbili kwa mwaka katika uchumi wa taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi hiyo, Dk. Albina Chuwa alisema ushirikiano ndiyo jambo la msingi katika kufikisha lengo na ndoto za watanzania, hivyo watajitahidi kutafuta fursa kupata matokeo mazuri.

“Ushirikiano wa kutosha ndiyo naomba kutoka kwa kila mmoja wetu, kwani haya yote tunayoyazungumza tutakuwa tunafanya kazi nyepesi katika kuhakikisha kituo chetu cha kaboni kinafanya vizuri,” alisema Dk. Albina.

Alieleza biashara ya kaboni inaendelea kukua kwa kasi duniani, hivyo bodi hiyo ina jukumu muhimu la kuhakikisha rasilimali za kaboni za Tanzania zinasimamiwa kwa uwazi, weledi na kuzingatia mifumo na viwango vinavyokubalika kimataifa.

Wajumbe wanaounda Bodi ya Kituo cha Kaboni ni Khamis Hamza Khamis, Amne Sued Kagasheki, Farhat Mabrouk, Dk. Ladislaus Kyaruzi, Rishad Bade pamoja na Dk. Philipina Shayo.

Previous Post

FCC, TCRA KUCHUNGUZA GHARAMA ZA BANDO NCHINI 

Next Post

SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

Next Post
SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

SALOME AIBANA KAMPUNI YA DONGFANG KWA KASI ISIYORIDHISHA MRADI WA UMEME MALAGARASI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. SAMIA AMLILIA ODINGA

DK. SAMIA AMLILIA ODINGA

6 months ago
RAIS DK. SAMIA AWATAKIA HERI WATANZANIA MIAKA 64 YA UHURU

RAIS DK. SAMIA AWATAKIA HERI WATANZANIA MIAKA 64 YA UHURU

4 months ago

Popular News

  • KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

    KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MUYUNGI ASISITIZA WANANCHI KUFANYA BIASHARA YA KABONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO BARAZA LA WAWAKILISHI YADHAMIRIA MAMLAKA YA VIPIMO ZANZIBAR IFIKIE VIWANGO VYA WMA BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • LAZARUS CHAKWERA AMALIZA ZIARA YA SIKIU 9 NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?