• ePaper
Sunday, May 17, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 12, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na NASRA KITANA

WAKATI kikosi cha Simba kikitarajiwa kushuka dimbani leo kupambana na Dodoma Jiji, kocha wa timu hiyo, Steve Barker amesema wamejipanga kupata ushindi.

Simba leo itawakaribisha Dodoma jiji katika mchezo wa wake wa 16 bora wa Kombe la Shirikisho(FA), utakaochezwa katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha saa 10:00 jioni.

Akizungumza kuelekea mchezo huo, Barker alisema pambano hilo litakuwa gumu kwa vile kila timu inahitaji kupata matokeo mazuri.

“Tumetoka kupata sare katika mechi iliyopita, tumefanyia kazi kasoro zote zilizojitokeza, hapa leng letu ni kupata ushindi.

“Pamoja na kushindwa kupata muda mzuri wa kufanya mazoezi lakini tumejitahidi kuondoa kasoro zote zilizokuwepo, tutapambana  kwa nguvu zote kupata ushindi na kusonga hatua inayofuata,” amesema.

Barker alifafanua kuwa wamefanyia kazi kasoro zote zilizojitokeza katika mechi zilizopita.

Kocha huyo aliwaomba mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kuwapa sapoti timu ishinde mchezo wa leo.

Nyota wa timu hiyo, Rushine De Reuck alisema wachezaji wote wa timu hiyo, wana morari ya kutosha kuelekea pambano hilo.

 “Tutaingia uwanjani kuhakikisha tunapambana kupata ushindi na kutumia vyema nafasi ambazo tutazipata, hatukuwa na matokeo mazuri hivyo hatutakubali kupoteza dhidi ya Dodoma Jiji,” alisema mlinzi huyo.

Naye kocha wa Dodoma Jiji, Aman Josiah alisema mechi dhidi ya Simba itakuwa ngumu lakini wao watahakikisha wanapata ushindi.

“Tumewaangalia wapinzani wetu vizuri na tumeona wapi kuna kasoro, hivyo tutahakikisha tunatumia udhaifu wa Simba kupata ushindi.

“Huu ni mchezo wa mtoano atakayefungwa anaondoka, nitakipanga vizuri kikosi changu kuhakikisha tunapata ushindi na kusonga mbele hatua inayofuata,” alisema kocha huyo.

Josiah alifafanua kuwa timu yake itaingia uwanjani katika pambano hilo, ikifahamu ni mchezo mgumu na wenye changamoto kubwa.

“Najua Simba hawajapata matokeo katika mechi mbili mfululizo hivyo watatumia mchezo huu ili kupata ushindi lakini sisi tumejipanga kupambana nao, kupata matokeo,” alisema Aman.

Mchezaji wa timu hiyo, William Edger alisema wachezaji wte wamejipanga vizuri kuelekea mchezo huo.

“Tunajua Simba ni timu bora hivyo tutaingia kwa kuwaheshimu na kucheza kwa nidhamu kubwa lengo ni kuhitaji ushindi na tutatumia kila mbinu ambazo mwalimu ametupatatia,” alisema William.

Nyota huyo amewaomba mashabiki na wapenzi wa timu yao kujaa kwa wingi uwanjani na kuwapa sapoti wafanye vizuri katika mchezo wa leo.

Previous Post

BONDIA NASRA, VENE WATOA SOMO LA AMANI

Next Post

RAIS YANGA AVUNJA UKIMYA KUHUSU  DAMARO

Next Post
RAIS YANGA AVUNJA UKIMYA KUHUSU  DAMARO

RAIS YANGA AVUNJA UKIMYA KUHUSU  DAMARO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

SERIKALI YATUMIA BILIONI 64/- KUBORESHA UWANJA WA NDEGE IRINGA

2 months ago
KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA 10 CBE

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA 10 CBE

2 months ago

Popular News

  • DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    DK. MWIGULU AHIMIZA WANANCHI KUIOMBEA AMANI YA NCHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA KITAIFA YA RAIS MSTAAFU MOGAE WA BOTSWANA, AKIMWAKILISHA RAIS DK. SAMIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DANGOTE AIPONGEZA SERIKALI, AANGAZIA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA NI NCHI YA PILI AFRIKA KUWA NA HADHI YA  UTALII WA JIOLOJIA (GEOPARK MUSEUM)

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAIPONGEZA PUMA ENERGY KWA MFUMO MPYA WA KIDIJITALI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?