• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

FCC, TCRA KUCHUNGUZA GHARAMA ZA BANDO NCHINI 

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 6, 2026
in Habari, Kitaifa
0
FCC, TCRA KUCHUNGUZA GHARAMA ZA BANDO NCHINI 
0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Dodoma
NA FRED ALFRED

TUME ya Ushindani (FCC) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), zinaendelea na uchunguzi kuhusu gharama za bando zinazotozwa na kampuni za mitandao ya simu kubaini kama wananchi wanarubuniwa.

Hayo yalibainishwa jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa FCC, Khadija Ngasongwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya serikali ya Awamu ya Sita ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Alisema uchunguzi utakaofanyika utatoa majawabu kama mlaji anaonewa au ni halali.

“Suala la bando za mitandao ni la kitaalamu ndiyo maana tuliona tufanye uchunguzi kwa kushirikiana na wenzetu wa TCRA ili tujue kama wananchi wanarubuniwa katika kupata huduma hizo,” alisema.

Aliongeza kuwa: ”Vilevile tunaendelea kushirikiana na Wakala wa Vipimo (WMA) kuangalia kiwango cha fedha kinachotozwa kinaendana na huduma anayopata ili kuthibitisha hayo kunahitaji uchunguzi wa kisayansi.”

BIDHAA BANDIA

Kuhusu udhibiti wa bidhaa bandia Khadija alisema FCC imeendelea kusimamia kikamilifu Sheria ya Alama za Bidhaa ambayo jukumu muhimu katika kuzuia uingizaji,

uuzaji na usambazaji wa bidhaa bandia au zile zenye maelezo potofu.

Alisema bidhaa bandia huzuia ushindani wa haki, kuathiri vibaya biashara halali na kuhadaa watumiaji, hivyo kuunda uwanja usio sawa wa biashara.

“Sheria hii inahakikisha kuwa biashara zinapewa fursa ya kufanikiwa kutokana na ubora, ubunifu na kufuata sheria, badala ya udanganyifu. Hii inakuza soko lenye ushindani wa haki na uwazi, likilinda imani ya watumiaji na kuwezesha makampuni kuwekeza kwa kujiamini katika ukuaji na ubunifu,” alisema.

Aliongeza kuwa:”Kudhibiti bidhaa bandia kwa mujibu wa sheria hii pia kunachangia ukuaji wa uchumi. Biashara halali zinabaki na mapato yake, jambo linalochochea uwekezaji zaidi, kuongeza ajira na kuendeleza ubunifu.”

Alisema jitihada za kuzuia bidhaa bandia zinaboresha sifa ya biashara kitaifa na kimataifa, kuwavutia wawekezaji na kuongeza mauzo ya nje.

“Kwa kuunganisha utekelezaji madhubuti, ushirikiano wa sekta, na uhamasishaji wa umma, sheria hii inahakikisha kuwa ushindani wa haki na uthabiti wa kisheria unachochea ukuaji wa uchumi endelevu wa nchi,” alisema.

KUMLINDA MTUMIAJI

Khadija alisema FCC imepanga kuendeleza juhudi za kumlinda mlaji dhidi ya mienendo potofu, hadaifu na kandamizi katika soko la bidhaa na huduma na kudhibiti bidhaa bandia.

Alisema katika kutekeleza hilo imeendelea kutatua malalamiko ya walaji, ambapo katika robo ya kwanza na ya pili malalamiko 63 yalishughulikiwa, kati ya malalamiko hayo 45 yalipatiwa ufumbuzi 19 yaliyobaki yapo katika hatua mbalimbali za utatuzi.

Pia alisema FCC ilisajili na kuthibitisha mikataba 27 inayoandaliwa na upande mmoja (SFCC), sanjari na kuandaa warsha na makongamano mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha inajenga uelewa kuhusu masuala ya kumlinda mlaji kwa wadau na mahusiano.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AIPA HESHIMA DIPLOMASIA YA TANZANIA

Next Post

MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO

Next Post
MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO

MASAUNI AZINDUA BODI YA KABONI, AIPA MAAGIZO MATANO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

AZAM FC,TRA UTD KAZI IPO

AZAM FC,TRA UTD KAZI IPO

3 months ago

“Wasichana milioni mbili wanufaika na elimu ya stadi za maisha

8 months ago

Popular News

  • KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

    KIGOGO CHAUMMA ‘AIPA TANO’ TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MUYUNGI ASISITIZA WANANCHI KUFANYA BIASHARA YA KABONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KAMATI YA UTALII, BIASHARA NA KILIMO BARAZA LA WAWAKILISHI YADHAMIRIA MAMLAKA YA VIPIMO ZANZIBAR IFIKIE VIWANGO VYA WMA BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • LAZARUS CHAKWERA AMALIZA ZIARA YA SIKIU 9 NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MAFANIKIO YA KISHINDO SGR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?