• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MAREKANI YAKOSHWA KASI MAENDELEO Z’BAR

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
March 24, 2026
in Habari, Kimataifa, Kitaifa
0
MAREKANI YAKOSHWA KASI MAENDELEO Z’BAR
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

MAREKANI imeipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kwa hatua kubwa ya maendeleo, hususan katika ujenzi wa miundombinu.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Balozi Andrew Lentz, alipokutana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, Ikulu Zanzibar.

Balozi Lentz alisema amefurahishwa na maendeleo ya Zanzibar hasa ujenzi wa miundombinu, akisema ni kipaumbele kwa nchi inayolenga kuvutia uwekezaji na kukuza uchumi.

Pia, Balozi Lentz aliahidi kupanua ushirikiano na Zanzibar katika sekta za afya, mabadiliko ya tabianchi, biashara na uwekezaji.

RAIS DK. MWINYI

Kwa upande wake Rais Mwinyi, alisema Zanzibar ina mipango na mikakati madhubuti kuhakikisha inajitegemea na kujitosheleza katika nishati ya mafuta na umeme, kuwa kituo kikuu cha usafirishaji kupitia bandari kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Rais Dk. Mwinyi alisema ujenzi wa Bandari Jumuishi ya Mangapwani, unatarajiwa kumaliza changamoto zilizopo na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa Zanzibar, ikiwemo mitambo ya megawati 200, matanki ya mafuta na bandari yenye uwezo wa kuhudumia meli kubwa ambayo itaondoa msongamano wa Bandari ya Malindi.

Alisema ukuaji wa sekta ya uwekezaji nchini na utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo, umeifanya Zanzibar kutafuta njia mbadala za kujitegemea katika nishati ya umeme, mafuta, gesi na kuleta mageuzi katika ujenzi wa Bandari ya Mangapwani.

Pia, aliihakikishia Marekani kuendeleza ushirikiano katika nyanja mbalimbali na kuishukuru kwa misaada yake kwa Tanzania, ikiwemo Zanzibar, akibainisha kuwa bado zipo fursa nyingi kwa kampuni na wawekezaji kutoka Marekani kuwekeza nchini.

BAADHI YA MIRADI

Katika kipindi cha Rais Mwinyi, barabara zimejengwa ikiwemo ujenzi wa flyover kutoka Mwanakwerekwe hadi Amani uliogharimu sh. bilioni 23.7 na Daraja la Uzi linalounganisha Unguja Ukuu na Kisiwa cha Uzi lenye urefu wa kilometa 2.2.

Pia, Rais Mwinyi amejenga miundombinu ya usafirishaji ya bahari, ukiwemo ujenzi wa Bandari ya Mangapwani, Bandari ya Fumba na Bandari ya Mpigaduli (Maruhubi).

Miradi mingine, Rais Mwinyi ametoa fedha za ujenzi wa shule mpya 60 zikiwemo 36 za ghorofa katika kila wilaya kwa lengo la kuondoa msongamano wa wanafunzi.

Pia, amejenga masoko makubwa kila wilaya yakiwemo Soko la Mwanakwerekwe, Jumbi, Mombasa na Chuini.

Katika hatua nyingine, Rais Mwinyi amelihakikishia Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kuwa SMZ itaendelea kushirikiana na shirika hilo katika kuimarisha huduma za mawasiliano Zanzibar.

Rais Dk. Mwinyi alisema hayo Ikulu, Zanzibar jana, alipokutana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTCL, David Nchimbi, aliyekwenda kujitambulisha.

Rais Mwinyi alisema sekta ya mawasiliano ni muhimu katika kukuza uchumi wa kidijitali, kuimarisha huduma za kijamii zikiwemo za elimu, afya ya mtandao na kuchochea uwekezaji wa utalii Zanzibar.

“Tutahakikisha tunaimarisha huduma za mawasiliano kwa sababu zinaleta tija katika kukuza uchumi,”alisema Rais Mwinyi.

Rais Mwinyi alisema mawasiliano imara ni yenye uhakika na yatakayongeza ufanisi wa shughuli za Serikali, biashara na huduma kwa wananchi.

Naye Mwenyekiti wa bodi hiyo, alimshukuru Rais Mwinyi kwa ushirikiano mzuri unaoendelea kati ya shirika hilo na SMZ.

Nchimbi alisema TTCL itaendelea kutoa huduma bora na za kisasa kwa kukidhi mahitaji ya wananchi na kuchochea maendeleo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano   (TEHAMA) nchini.

Alimweleza Rais Mwinyi kuimarika mawasiliano Zanzibar, kutaleta manufaa makubwa kwa TTCL, yakiwemo kupanua wigo wa soko, kuongeza idadi ya wateja wa huduma za intaneti, mawasiliano ya simu na kukuza mapato ya shirika.

Previous Post

WADAU WAUNGA MKONO MSISITIZO WA RAIS DK. SAMIA KUHUSU MAADILI

Next Post

TANZANIA INAYO HIFAHI YA KUTOSHA YA MAFUTA

Next Post
TANZANIA INAYO HIFAHI YA KUTOSHA YA MAFUTA

TANZANIA INAYO HIFAHI YA KUTOSHA YA MAFUTA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

DK. NCHIMBI : KUMBUKIZI ZA MAJIMAJI ZIWE CHACHU YA UZALENDO NA UWAJIBIKAJI

DK. NCHIMBI : KUMBUKIZI ZA MAJIMAJI ZIWE CHACHU YA UZALENDO NA UWAJIBIKAJI

2 months ago
MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

MAWAZIRI SABA NA MIKAKATI YA KAZI

5 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?