Na MWANDISHI WETU
WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tamasha la mtoko na Christina Shusho litakalofanyika wakati wa Sikukuu ya Pasaka.
Tamasha hilo, limepangwa kufanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam, msanii wa muziki wa injili, Christian Shusho alisema tamasha hilo halitakuwa na kiingilio.
“Tamasha hili, kutakuwa na waimbaji mbalimbali kutoka nje ya nchi na ndani ya nchi kwa ajili kutumbuiza siku hiyo,” amesema.
Alifafanua kuwa tamasha hilo litashirikisha wasanii hao ili kutumbuiza na kuabudu Mungu siku ya sikukuu hiyo.
“Wasanii mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi watakuwepo katika tamasha hilo akiwemo Rose Muhando, Joel Lwaga, Bella Kombo, Paul Clement na wengine wengi ambao wanafanya vizuri katika muziki wa injili,” alisema.
Msanii huyo alitoa wito kwa watu mbalimbali kujitokeza kwa wingi siku ya tamasha hilo kwenda kushuhudia burudani nzuri ya muziki na kuabudu Mungu kwa pamoja ndani ya Sikukuu ya Pasaka.




