• ePaper
Thursday, April 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

CHAMUDATA YAZUNGUMZIA AMANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 4, 2026
in Habari, Kitaifa
0
CHAMUDATA YAZUNGUMZIA AMANI
0
SHARES
7
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na AMINA KASHEBA

UONGOZI wa Chama Cha Muziki wa Dansi Tanzania (CHAMUDATA), umewataka Watanzania kudumisha amani ya nchi kwani ndiyo nguzo muhimu ya kukuza siasa, uchumi na michezo.

Kauli hiyo, imetolewa jijini Dar es Salaam na Makamu Mwenyekiti wa CHAMUDATA, Angel Bushoke alipozungumza na UHURU kuwa lengo la kufanya hivyo ni kuiunga mkono serikali.

“Unajua serikali yetu inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  inafanya mambo mengi makubwa,  inapambana kwa nguvu zote kuhakikisha taifa linakuwa na amani, hivyo watanzania wanapaswa kuungana na kuwapuuza watu wenye kutaka vurugu,”alisema.

Angel alifafanua kuwa viongozi wa CHAMUDATA wana imani kubwa na i Tume Huru ya Uchunguzi ya Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu. uliofanyika Oktoba 29, mwaka jana.

 Rais Dk. Samia aliunda tume hiyo, Novemba 18, mwaka jana kwa mujibu wa Sheria ya Tume za Uchunguzi ya mwaka 2023 (Sura ya 32) ambapo tume hiyo inaongozwa na Mwenyekiti, Jaji Mkuu Mstaafu, Mohamed Chande Othman.

“Tuseme kweli nchi ikiwa haina amani hakuna jambo litakalo fanyika, hivyo wananchi tunapaswa kushikamana na kama zipo changamoto zitatuliwe kwa hoja na si fujo.

“Wito wangu kwa Watanzania ni vyema tukaendelea kudumisha amani ya nchi yetu maana Tanzania tunasifika kuwa wakarimu ndiyo maana kuna baadhi ya watu wanatoka nchi zao na kuja hapa kwetu kuwekeza,” alisema.

Makamu Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa siku zilizopita zipo baadhi ya timu ziliomba kuja kucheza michezo yao hapa nchini kutokana na nchi zao kukosa amani.

“Hakuna jambo zuri kuona nchi yetu mwakani inakuwa moja ya  nchi waandaji wa michuano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2027, hii yote imetokana na kuwepo utulivu na amani,”alisema.

Previous Post

MCHENGERWA ASHUSHA MAAGIZO KWA WAGANGA WAKUU WA MIKOA, WILAYA

Next Post

RAIS DK. SAMIA SULUHU MWANADEMOKRASIA WA KISIASA

Next Post
RAIS DK. SAMIA SULUHU MWANADEMOKRASIA WA KISIASA

RAIS DK. SAMIA SULUHU MWANADEMOKRASIA WA KISIASA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

TANZANIA NA CHINA ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIMKAKATI

4 months ago
DK. SAMIA AAHIDI NEEMA ZAIDI GAIRO

DK. SAMIA AAHIDI NEEMA ZAIDI GAIRO

8 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?