• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

CHOBWEDO ATIKISA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 11, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
CHOBWEDO ATIKISA
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU, Arusha

BAADA ya kufanya vizuri, winga wa TRAUnited, Ramadhan Chobwedo amezitikisa timu za Simba na Yanga na kuanza kumfuatilia.

Taarifa iliyopatikana, imeeleza kuwa  nyota huyo inasemakana tayari ameingia mkataba wa awali na klabu ya Simba.

Simba juzi iliambulia suluhu katika mchezo wake wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Baada ya kumalizika pambano hilo, inasemekana viongozi wa Simba walifanikiwa kumpatia mkataba wa awali mchezaji huyo lengo likiwa ni kuitumikia timu hiyo msimu ujao.

“Chobwedo tayari amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa awali kujiunga na Simba baada ya msimu huuutakapomalizika,”alisema kiongozi moja wa Wekundu wa Msimbazi ambaye hakupenda kutajwa jina lake.

Alipoulizwa Meneja wa Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally alisema Chobwedo ni mchezaji mzuri na kila timu inatamani kuwa naye.

Aliongeza kuwa kama kocha wao, Steve Barker atampendekeza basi viongozi watafanya mazungumzo  ya kumsajili.

“Ni mchezaji mzuri na mwenye nguvu kila timu inatamani kuwa na mchezaji kama huyo, lakini niwaambie tu kuwa hawatasajili mchezaji yeyote hadi mwalimu wao Steve Barker atakapotoa mapendekezo,” alisema Ahmed.

Lakini taarifa zaidi zimeeleza kuwa mchezaji huyo anafuatiliwa na Yanga ambapo juzi walituma watu wao kuangalia kiwango cha nyota huyo.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa Yanga nao jana usiku walikuwa wanajaribu kuzungumza na Chobwedo.

Awali imedaiwa kuwa Chobwedo alikuwa anatembea na mkataba wa Singida BS.

Ofisa Habari wa TRA, Christina Mwagala alipoulizwa alisema mawazo yao yapo kwa ajili ya mchezo dhidi ya Namun go FC wa Kombe la FA.

“Mambo ya usajili muda wake bado, nafahamu Chabwedo bado mchezaji wetu, hivi sasa tunaangalia safari ya kwenda Ruangwa kucheza na Namungo FC,”alisema kwa ufupi kiongozi huyo.   

Wakatihuohuo, ChobwedoalisemakuwaSimba ina bahati kwani walijipanga kuifunga katika mchezo wao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao jijini Arusha, alisema kila mchezaji alipenda kushinda mchezo huo lakini imekuwa bahati mbaya.

“Simba wana bahati sana, tulijipanga vizuri kuwafunga, lakini wana bahati kwa vile tumewakosa, bao letu lilikataliwa,” alisema.

Hata hivyo, mchezaji huyo wa TRA amesema ana imani timu yao itaendelea kufanya vizuri kutokana na kikosi imara walicho nacho.

Pia, amekiri kuwa ligi hiyo ni ngumu kutokana na timu nyingi kujipanga vizuri msimu huu.

“Ukweli ligi yetu ni ngumu, kila timu inapenda kufanya vizuri, mara nyingi zikiwa nyumbani,”alisema Chobwedo.

Previous Post

KOCHA SIMBA ACHEFUKWA

Next Post

MSANII CECY AHIMIZA AMANI

Next Post
MSANII CECY AHIMIZA AMANI

MSANII CECY AHIMIZA AMANI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MATOKEO YAMSIKITISHA KOCHA YANGA

MATOKEO YAMSIKITISHA KOCHA YANGA

2 months ago
MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

MAELFU YA WAGONJWA KUTOKA NJE YA NCHI WAMIMINIKA KUPATA HUDUMA

1 month ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?