• ePaper
Saturday, May 30, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

BONDIA NASRA, VENE WATOA SOMO LA AMANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
April 11, 2026
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
BONDIA NASRA, VENE WATOA SOMO LA AMANI
0
SHARES
18
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ZIANA BAKARI

BONDIA Nasra Msami, amewahimiza vijana kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani kwa kuepuka kushawishiwa na mtu yeyote kuvuruga amani ya nchi.

Akizungumza na UHURU Dar es Salaam , bondia huyo alisema vijana wana nafasi kubwa ya kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na utulivu kupitia maamuzi sahihi na ushiriki wao katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Aliwasisitiza vijana kuwa ni muhimu kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa sheria na badala yake wajikite katika kazi halali zinazowajenga kiuchumi.

“Vijana wakifanya hivyo watasaidia kujenga taifa lenye mshikamano na maendeleo endelevu, hivyo niwaombe kuzingatia hili kwa umakini.

“Amani ni msingi wa mafanikio katika kila sekta, hivyo kila kijana ana wajibu wa kuilinda tunu ya taifa, bila amani, hata juhudi za maendeleo zinapotea,” alisema.

Pia, bondia huyo aliwasihi vijana kuwa mfano mzuri katika jamii kwa kuhubiri upendo, mshikamano na uvumilivu, ili kuimarisha umoja wa kitaifa.

Naye Patricia Nyamaka anayefahamika zaidi kwa mashabiki zake kwa jina la ‘Vene’ katika tamthilia ya ‘Kombolela’ msimu wa pili, amewasihi wasanii wenzake kuwa mabalozi wa kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa amani nchini.

Msanii huyo amesema sanaa ina nguvu kubwa ya kufikisha ujumbe kwa watu wa rika zote.

“Nawaomba wasanii wenzangu, tuna wajibu wa kuelimisha jamii kuhusu amani, kupitia muziki, maigizo, filamu na sanaa nyingine,”alisema.

Aliongeza kuwa wasanii wanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuimarisha mshikamano na upendo miongoni mwa wananchi.

“Wasanii tunapaswa kutumia majukwaa yetu kuhamasisha amani na kuepuka maudhui yanayoweza kuchochea migogoro au chuki katika jamii.

“Kila msanii ana kazi hiyo  kwa nguvu zote, kwa mashabiki zake, amani ni msingi wa maendeleo ya sekta zote, ikiwemo sekta ya sanaa, hivyo wasanii wanapaswa kuilinda kwa nguvu zote,” alisema.

Alieleza kuwa bila amani, hata ubunifu na vipaji vya wasanii haviwezi kuonekana.

Previous Post

WADAU WANA MATARAJIO CHANYA NA TUME YA JAJI CHANDE

Next Post

 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

Next Post
 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

 KOCHA SIMBA AITISHA DODOMA JIJI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CHAMBUA: DUBE KAMA MAYELE

CHAMBUA: DUBE KAMA MAYELE

6 months ago
RAIS DK. SAMIA APOKELEWA NA WATUMISHI IKULU

RAIS DK. SAMIA APOKELEWA NA WATUMISHI IKULU

7 months ago

Popular News

  • RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    RAS: UTUNZAJI MAZINGIRA AJENDA YA KIPAUMBELE KWA MKOA WA MWANZA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • UPELE UMEPATA MKUNAJI STARS

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‎ RAIS DK. SAMIA: POLISI MSIDHARAU TAARIFA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • DK. MWIGULU ATETA NA WAZIRI MKUU WA CONGO BRAZZAVILLE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MASTAA YANGA WAUTAJA UBINGWA LIGI KUU BARA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?