• ePaper
Thursday, May 14, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

TANZANIA YANG’ARA KWA UDHIBITI MAAFA SADC

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 14, 2026
in Habari, Kitaifa
0
TANZANIA YANG’ARA KWA UDHIBITI MAAFA SADC
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI MAALUMU, Zimbabwe

TANZANIA imeendelea kung’ara katika ukanda wa Kusini mwa Afrika baada ya kutajwa kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mifumo madhubuti ya usimamizi wa maafa, hatua inayozifanya nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kujifunza kupitia uzoefu wake.

Hayo yalielezwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kaspar Mmuya kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Profesa Palamagamba Kabudi wakati wa Mkutano wa Sita wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri Wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa nchi wanachama wa SADC uliofanyika mjini Masvingo, Zimbabwe, juzi.

Amesema Tanzania imefanikiwa kuimarisha mifumo ya kuzuia, kupunguza madhara, kujiandaa na kurejesha hali baada ya maafa kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya uratibu wa maafa nchini.

Kwa mujibu wa Mmuya, moja ya mafanikio makubwa ni kuanzishwa Kituo cha Ufuatiliaji wa Mwenendo wa Majanga na Tahadhari ya Mapema ambacho kinafanya kazi muda wote kufuatilia na kuchambua taarifa za majanga.

“Kwa kupitia kituo hiki, serikali imepata taarifa za mapema kuhusu majanga yanayoweza kutokea, kufanya uchambuzi wa madhara na kuweka mikakati ya haraka ya kukabiliana nayo,” alisema Mmuya.

Ameongeza matumizi ya teknolojia ya kisasa katika ukusanyaji na uchambuzi wa takwimu za wakati halisi yamechangia kuongeza ufanisi na kurahisisha utoaji wa taarifa rasmi kwa wananchi kuhusu namna ya kujiandaa dhidi ya maafa.

“Tunatumia takwimu za sasa na za zamani kutabiri hatari zinazoweza kujitokeza, jambo ambalo linaisaidia serikali kupanga kwa usahihi hatua za kurejesha hali na kuendelea kulinda maisha ya wananchi,” alielez.

Aidha, amewaalika wajumbe kutoka nchi za SADC kutembelea Tanzania kujionea namna mifumo hiyo inavyofanya kazi pamoja na ubunifu unaotumika katika usimamizi wa maafa.

Mkutano huo wa siku nne umezikutanisha nchi 16 wanachama wa SADC pamoja na wataalamu wa kitaifa na mashirika ya kimataifa kujadili utekelezaji wa programu za kikanda za usimamizi wa maafa na namna ya kuimarisha ushirikiano wa kikanda.

Pamoja na mambo mengine, mkutano huo unatarajiwa kuwa jukwaa muhimu kwa mawaziri na washirika wa maendeleo kujadili uwekezaji katika sekta ya usimamizi wa maafa kwa lengo la kujenga ustahimilivu wa kikanda dhidi ya majanga yanayoendelea kujitokeza duniani.

Previous Post

POLISI WAPATA SEHEMU YA KICHWA CHA JAMES TEMBA, MGANGA WA KIENYEJI MBARONI

Next Post

WADAU AFYA WAKUTANA KUSAKA MWAROBAINI WA MADENI MSD

Next Post
WADAU AFYA WAKUTANA KUSAKA MWAROBAINI WA MADENI MSD

WADAU AFYA WAKUTANA KUSAKA MWAROBAINI WA MADENI MSD

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

MWIGULU ATAJA MWAROBAINI MAFURIKO DARAJA LA DUMILA

6 days ago
MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA AFYA

MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA AFYA

2 days ago

Popular News

  • TANZANIA, KENYA WAJADILI KUIMARISHA NJIA ZA UMEME

    TANZANIA, KENYA WAJADILI KUIMARISHA NJIA ZA UMEME

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WADAU AFYA WAKUTANA KUSAKA MWAROBAINI WA MADENI MSD

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TANZANIA YANG’ARA KWA UDHIBITI MAAFA SADC

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • POLISI WAPATA SEHEMU YA KICHWA CHA JAMES TEMBA, MGANGA WA KIENYEJI MBARONI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BEHEWA LA AFYA LAIBUA WADAU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?