• ePaper
Thursday, May 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home AFYA

DK. YONAZI APOKEA TAARIFA AFUA ZA UKIMWI PWANI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
May 18, 2026
in AFYA, Habari, Kitaifa
0
DK. YONAZI APOKEA TAARIFA AFUA ZA UKIMWI PWANI
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dk. Jim Yonazi, amepokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Pwani katika utekelezaji wa afua za masuala ya UKIMWI, hasa huduma na mipango inayohusu Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU).

Dk. Yonazi amepokea taarifa hiyo leo Mei 18, 2026 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, baada ya kutembelea, kukagua na kutoa elimu katika Kituo cha Maarifa cha Mdaula kilichopo Chalinze, mkoani humo.

RC Kunenge amemweleza katibu huyo kuwa, serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wamechukua hatua ya kuboresha huduma za afya na ustawi wa jamii kwa wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa kutoka kwa RC Kunenge, Dk. Yonazi amesema serikali imeongeza bajeti katika huduma za VVU na UKIMWI ili kuleta ufanisi zaidi katika utoaji wa huduma.

Zahanati ya Mdaula ilianza kutoa huduma za afya Oktoba 2022, zikiwemo huduma za wagonjwa wa nje, huduma za mama na mtoto, uzazi na chanjo kupitia kliniki tembezi.

Previous Post

WASIRA: WALIOFANYA VURUGU WAPATIKANE

Next Post

RAIS DK. SAMIA ATOA AGIZO  KOMBE LA DUNIA 2026

Next Post
RAIS DK. SAMIA ATOA AGIZO  KOMBE LA DUNIA 2026

RAIS DK. SAMIA ATOA AGIZO  KOMBE LA DUNIA 2026

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO

CCM YAOMBOLEZA KIFO CHA KARDINALI PENGO

3 months ago
DK. MWINYI: MEMA YA MFUNGO WA RAMADHANI YAENDELEZWE

DK. MWINYI: MEMA YA MFUNGO WA RAMADHANI YAENDELEZWE

2 months ago

Popular News

  • MWANZO, MWISHO SIMULIZI MAUAJI YA MCHINA DAR

    MWANZO, MWISHO SIMULIZI MAUAJI YA MCHINA DAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUDUMISHA SERA YA CHINA MOJA NA KUIMARISHA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, COASTAL HAPATOSHI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RIO USIPIME KABISA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. SAMIA AWAPA TABASAMU WAPIGANAJI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?