Na MWANDISHI WETU
KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dk. Jim Yonazi, amepokea taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Pwani katika utekelezaji wa afua za masuala ya UKIMWI, hasa huduma na mipango inayohusu Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU).
Dk. Yonazi amepokea taarifa hiyo leo Mei 18, 2026 kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, baada ya kutembelea, kukagua na kutoa elimu katika Kituo cha Maarifa cha Mdaula kilichopo Chalinze, mkoani humo.
RC Kunenge amemweleza katibu huyo kuwa, serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wamechukua hatua ya kuboresha huduma za afya na ustawi wa jamii kwa wananchi wa mkoa huo.
Akizungumza baada ya kupokea taarifa kutoka kwa RC Kunenge, Dk. Yonazi amesema serikali imeongeza bajeti katika huduma za VVU na UKIMWI ili kuleta ufanisi zaidi katika utoaji wa huduma.
Zahanati ya Mdaula ilianza kutoa huduma za afya Oktoba 2022, zikiwemo huduma za wagonjwa wa nje, huduma za mama na mtoto, uzazi na chanjo kupitia kliniki tembezi.




