• ePaper
Sunday, July 26, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
July 24, 2026
in Habari, Kitaifa
0
MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR
0
SHARES
5
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Zanzibar

Na HANIFA RAMADHANI

ZANZIBAR ni neema tu! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi kuzindua mabasi yanayotumia umeme hatua inayolenga kupunguza uchafunzi wa mazingira na kuimarisha matumizi ya nishati safi.

Dk. Mwinyi amesema uzinduzi huo ni mkakati wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuiwezesha Zanzibar kuwa kinara kwa matumizi ya usafiri wa magari yanayotumia umeme.

Akizindua huduma za usafiri huo wa umma na kituo cha mabasi hayo, Dk. Mwinyi alisema utekelezaji wa mpango huo ni sehemu ya mkakati wa serikali kuhamasisha matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira, kupunguza utegemezi wa mafuta na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Alisema matumizi ya vyombo vinavyotumia umeme yataongeza ufanisi wa sekta ya usafiri na kuiwezesha Zanzibar kuwa mfano bora wa matumizi ya nishati mbadala Afrika Mashariki.

Alibainisha kuwa, hatua hiyo ni mwendelezo wa mkakati wa serikali kubadilisha vyombo vya usafiri wa umma kutoka kutumia mafuta kwenda umeme, hivyo alihimiza sekta binafsi kuinga mfano huo.

“Leo (jana) nimefurahi kupata fursa ya kuweka historia ya kuanzisha vyombo vya usafiri wa umma vinavyotumia umeme na muda mfupi ujao, tutaendeleza hatua hizi ili njia zote nchi nzima ziwe na vyombo vinavyofanana na hivi tunavyovizindua,” alisema.

Aidha, alisema ufunguzi wa kituo hicho ni mwendelezo wa jitihada za serikali kuimarisha haiba ya mji wa Zanzibar na kutoa huduma bora za usafiri kwa wananchi.

Dk. Mwinyi alibainisha kuwa, mradi huo ni mwanzo wa mambo makubwa yanayotarajiwa kumiminika visiwani humo na kuahidi kuendelea kuboresha usafiri wa umma unaotumia umeme.

“Tuliadihi teksi za baharini, treni zinakuja, hivyo wale ambao wana fitina, husda kwa kauli tunazozitoa nawaambia kwamba tumeshajipanga katika utekelezaji na ndiyo maana tunatembea kifua mbele.

“Mabasi yanaonekana, vituo vinaendelea kujengwa na tutaendelea kutekeleza ahadi zetu tulizozitoa ili Zanzibar ibadilike katika nyanja zote,” alisema.

Aliutaka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kuhakikisha vituo vinavyoendelea kujengwa vikamilike kwa wakati wananchi na wageni wanufaike na huduma hiyo.

Alitumia nafasi hiyo kuwapongeza wahusika wa mradi huo kuweka viwango maalumu vya nauli hususan kwa wazee wastaafu na wanafunzi.

Rais Mwinyi aliwasihi wananchi kuendelea kuiunga mkono serikali na kuwa walinzi wa miundombinu iendelee kuleta maendeleo hususan katika sekta ya usafiri.

ZANZIBAR KUBADILIKA KIUCHUMI

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Juma Malik Akil, alisema mradi huo ni utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Nane inayongozwa na Dk. Mwinyi kuibadilisha Zanzibar kiuchumi.

Previous Post

KOCHA AIPA JEURI YANGA

Next Post

KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

Next Post
KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

NECTA : TUMETOA MATOKEO KWA NAMBA KULINDA TAARIFA BINAFSI ZA WANAFUNZI

9 months ago
MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

MAKONDA WEMBE ULE ULE AFCON

6 months ago

Popular News

  • KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    KATIBA MSINGI WA HAKI – DK. NCHIMBI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MABASI YA UMEME REKODI ZANZIBAR

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KOCHA AIPA JEURI YANGA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • MWALIMU, GUEYE WAPO SIMBA SANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI ASHTUKIA ‘USANII’ WA WACHIMBAJI MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Not enough quota to unlock this post
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?