• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

KIKWETE AWATOLEA UVIVU WAZUSHI, ASEMA UTEUZI WA DK. SAMIA ULIFUATA KATIBA YA CCM

admin by admin
August 28, 2025
in Habari, Kitaifa, Uchaguzi
0
KIKWETE AWATOLEA UVIVU WAZUSHI, ASEMA UTEUZI WA DK. SAMIA ULIFUATA KATIBA YA CCM
0
SHARES
36
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

NA MUSSA YUSUPH

RAIS Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete, amewatolea uvivu wanaopotosha kwa kudai kwamba uteuzi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) haukufuata Katiba ya chama hicho.

Akihutubia maelfu ya wanachama wa CCM katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika Uwanja wa Tanganyika Packers, jijini Dar es Salaam, Dk. Kikwete alisema mchakato huo umefuata utaratibu wa chama ambao pia ulitumika kwa marais waliopita walipotaka kugombea awamu ya pili.

“Hao wanaosema huenda hawafahamu utaratibu wa chama, au wanajifanya hamnazo.

Tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanza, ndani ya CCM tuna utaratibu kwamba Rais aliyepo madarakani akimaliza kipindi cha kwanza anapewa nafasi ya kuendelea awamu nyingine.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Mkapa, kwangu na Magufuli.

Kwanini iwe nongwa kwa Samia?” alihoji huku akishangiliwa na umati wa wananchi.

Dk. Kikwete alibainisha kuwa mwangwi wa kauli mbiu ya “Samia mitano tena” ulitokana na azimio la mkutano mkuu wa CCM mapema mwaka huu, baada ya wajumbe kuridhishwa na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho chini ya uongozi wa Rais Dkk. Samia.

Alisema Dk. Samia alipokea nchi katika kipindi kigumu baada ya kifo cha Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli, ambapo hofu ilitanda juu ya hatma ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo.

Hata hivyo, alisema baada ya miaka minne Rais Dk. Samia amedhihirisha uwezo, ubunifu na maono ya mbali katika kuliongoza taifa.

Kikwete alitaja falsafa ya 4R, usimamizi wa mahusiano ya kidini, kuimarisha haki za binadamu na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo elimu, afya na miundombinu kama mifano ya mafanikio ya Rais Samia.

Aliongeza kuwa matumizi ya fedha za UVIKO-19 kugusa moja kwa moja maisha ya wananchi ni uthibitisho wa ubunifu na uongozi wenye kulenga maendeleo ya watu.

Alisisitiza kuwa CCM kimeweka utaratibu wake na ni muhimu heshima ikatolewa kwa taratibu hizo, huku akihitimisha kuwa kauli mbiu ya chama “Kazi na Utu, Tunasonga Mbele” ni kielelezo cha dhamira ya Rais Samia katika kuendeleza taifa.

Previous Post

DK. NCHIMBI ATOA AHADI KWA DK. SAMIA

Next Post

WASIRA : DK. SAMIA ANASTAHILI ‘MITANO TENA’

Next Post
WASIRA : DK. SAMIA ANASTAHILI ‘MITANO TENA’

WASIRA : DK. SAMIA ANASTAHILI ‘MITANO TENA’

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WACHEZAJI WA TEMBO WARRIORS

TEMBO WARRIORS KUFANYIWA MCHUJO

8 months ago
GAMONDI AITA JESHI LA MAANGAMIZI, MANULA NDANI

GAMONDI AITA JESHI LA MAANGAMIZI, MANULA NDANI

4 weeks ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?