• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. MWINYI AONYA SIASA ZA CHUKI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
September 6, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uchaguzi
0
RAIS DK. MWINYI AONYA SIASA ZA CHUKI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi

0
SHARES
3
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na HANIFA RAMADHANI,

Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewaomba viongozi wa dini, kupaza sauti kuwakumbusha wanasiasa kuacha kuhubiri siasa za chuki, mifarakano, ubaguzi na matusi hususan kipindi cha kampeni.

Dk. Mwinyi, ameyasema hayo mjini Unguja katika kongamano la baraza la Maulid Zanzibar, lililofanyika ukumbi wa Polisi Ziwani, mjini Unguja.

Amesema yapo maneno yameanza kutolewa na baadhi ya viongozi wa siasa, yanayoashiria uvunjifu wa amani, hivyo ni wajibu wao, kukemea kauli hizo ambazo zinaweza kuipeleka nchi pabaya.

Aidha, amesema siyo vyema kulinyamazia jambo hilo kwa kuwa kuvunjika amani, hakuanzi na bunduki, bali huanza na viashiria vikiwemo vitisho kutoka kwa baadhi ya wanasiasa.

“Tuendelee kufanya hivyo, wanaohimizwa kutoka kwenda kuvunja amani, wasikubali maana haitakuwa faida yoyote,” amesema.

Dk. Mwinyi, amesema ni wajibu wa kila mmoja kuwa mstari wa mbele, kuilinda amani kabla na baada ya uchaguzi kwa kujiepusha na kila kitu kitakachovunja amani.

“Viongozi wa dini, wananchi, masheikh, wanahabari na viongozi wa siasa, tujitahidi kuwa walinzi wa amani yetu na kuhakikisha, kila mmoja anahubiri hilo, tujiepushe na viashiria vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani katika nchi yetu,” amesema.

Amebainisha kuwa, taifa lolote, haliwezi kuwa salama wala kuendelea bila amani, hiyo inaonesha wazi amani ni moyo wa mafanikio ya mtu na jamii kwa ujumla.

“Haya ameyathibitisha Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kitabu chake kitukufu cha Quraan kwa aya mbalimbali na kusisitizwa na kuhimizwa katika hadithi za Mtume Muhamad (S.A.W),” amesema.

Akizungumzia mada zilizowasilishwa katika kongamano hilo, vikiwemo viashiria vya uvunjifu wa amani, amesema zinaendana na wakati uliopo kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Amesema kongamano hilo, limeakisi moja kwa moja hali halisi ya taifa na haja ya kudumisha amani ili wazidi kupiga hatua za maendeleo na kupita salama katika kipindi cha uchaguzi.

“Nimefarijika kuona wengi wetu tunazugnumza kauli moja ya kuhimiza amani katika taifa, hatua hiyo ni dalili ya kila mmoja wetu kutambua umuhimu wa kuienzi na kuidumisha neema hii ambayo ni msingi wa mafanikio,” amesisitiza.

Waziri wa Nchi, Ofi si ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Dk. Haroun Ali Suleiman, amewasisitiza waumini kufuata mafundisho na maamrisho ya Mwenyezi Mungu na kuacha makatazo ya Mwenyezi Mungu.

Awali, Katibu Mtendaji Ofi si ya Mufti Zanzibar, Sheikh Khalid Ali Mfaume, amesema maadhimisho ya kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW), lazima yaingizwe katika maisha ya kila siku kwa kuwa kutofanya hivyo ni kwenda kinyume na maamrisho na mafundisho mema.

Amempongeza Dk. Mwinyi kwa kulisimamia jambo hilo na amekuwa mfano katika uongozi wake na watu wengine wanatakiwa kujifunza kwake. Mwenyekiti wa Baraza la Maulid Zanzibar, Abubakar Mohammed Mussa, amesema shughuli hiyo sio ya kujijenga kiimani tu bali pia imelenga kuendeleza utamaduni wa Uislaam na jamii katika mazazi ya Mtume Muhammad (S.A.W).

Previous Post

DK. NCHIMBI AWAAHIDI FURSA WACHIMBAJI WADOGO

Next Post

WASIRA AVUNJA MAKUNDI CCM ARUSHA, MANYARA

Next Post
WASIRA  AVUNJA MAKUNDI CCM ARUSHA, MANYARA

WASIRA AVUNJA MAKUNDI CCM ARUSHA, MANYARA

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WABUNGE WATEULE KUWASILI DODOMA KUANZIA NOVEMBA 8 -10

WABUNGE WATEULE KUWASILI DODOMA KUANZIA NOVEMBA 8 -10

5 months ago
YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

YANGA, SIMBA NI VIKUMBO

4 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?