• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

WABUNGE WATEULE KUWASILI DODOMA KUANZIA NOVEMBA 8 -10

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 5, 2025
in Habari, Kitaifa, Siasa, Uncategorized
0
WABUNGE WATEULE KUWASILI DODOMA KUANZIA NOVEMBA 8 -10
0
SHARES
11
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na MWANDISHI WETU

DODOMA

BUNGE limewatangazia wabunge wote wateule kuwasili Dodoma kuanzia Novemba nane hadi 10 mwaka huu, kwa ajili ya usajili na shughuli mbalimbali za kiutawala kabla ya kuanza kwa mkutano wa kwanza wa Bunge la 13.

Kwa mujibu wa Tangazo la Rais katika Gazeti la serikali Toleo Maalumu Na. 11 la Novemba nne mwaka huu, mkutano wa kwanza wa Bunge jipya utafanyika Novemba 11 mwaka huu.

Aidha, taarifa iliyotolewa jijini Dodoma na Katibu wa Bunge, Baraka Leonard imeeleza kuwa, miongoni mwa shughuli zitakazofanyika katika mkutano huo ni kusomwa kwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge, uchaguzi wa Spika, kiapo cha uaminifu kwa wabunge wote na uthibitisho wa uteuzi wa Waziri Mkuu.

Taarifa hiyo imeeleza shughuli nyingine zitakazofanyika ni uchaguzi wa Naibu Spika pamoja na ufunguzi rasmi wa Bunge Jipya utakaoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Vilevile, wabunge wateule wametakiwa kuvaa mavazi rasmi, huku wakiwa na nyaraka muhimu ikiwemo Hati ya Kuchaguliwa, Kitambulisho cha Taifa, Kadi ya Benki, vyeti vya elimu na wasifu binafsi (CV).

Kwa wabunge walio katika ndoa, wanatakiwa kuwasilisha cheti halisi cha ndoa, huku wazazi wakitakiwa kuja na vyeti vya kuzaliwa vya watoto walio chini ya miaka 21.

Pia, utaratibu wa uchaguzi wa Spika na Naibu Spika umetangazwa rasmi kupitia matangazo Na. 14824A na 14824B katika Gazeti la Serikali, ukielekeza namna wagombea watakavyopendekezwa na kupigiwa kura ndani ya Bunge.

Previous Post

RAIS DK. SAMIA AKABIDHIWA NYARAKA ZA KAZI

Next Post

KIDATO CHA PILI KUANZA MITIHANI NOVEMBA 10

Next Post
KIDATO CHA PILI KUANZA MITIHANI NOVEMBA 10

KIDATO CHA PILI KUANZA MITIHANI NOVEMBA 10

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

TUZO YA CAF KWA RAIS DK. SAMIA NI HESHIMA

TUZO YA CAF KWA RAIS DK. SAMIA NI HESHIMA

5 months ago
TRILIONI 1.7/- ZANUFAISHA MIRADI MKOANI SINGIDA

TRILIONI 1.7/- ZANUFAISHA MIRADI MKOANI SINGIDA

7 months ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?