• ePaper
Tuesday, April 21, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

KIPA CAMARA APASULIWA GOTI

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 20, 2025
in Burudani, Habari, Kitaifa, Michezo
0
KIPA CAMARA APASULIWA GOTI
0
SHARES
4
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na VICTOR MKUMBO

KIPA namba moja wa Simba, Moussa Camara amefanyiwa upasuaji wa goti na umekwenda vizuri.

Kipa huyo alifanyiwa upasuaji wa goti nchini Morocco ambapo anatarajiwa kukaa nje ya dimba kwa kipindi cha kati ya wiki nane hadi 10.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally alisema Camara amefanyiwa upasuaji wa goti na imekwenda vizuri.

“Camara amefanyiwa upasuaji wa goti nchini Morocco na umekwenda vizuri, tunatarajia kumkosa katika kipindi kisichopungua wiki nane hadi 10.

“Tunawaomba Watanzania na mashabiki wa Simba kuendelea kumwombea dua kuhakikisha anarejea katika hali yake ya kawaida na kurudi katika majukumu yake ndani ya Simba,” alisema.

Ahmed alisema Camara alifanyiwa upasuaji wa goti na madaktari bingwa nchini Morocco.

“Tuna imani kipa wetu atarejea dimbani kwa wakati akiwa fiti baada ya kupona majeraha yanayomkabili,”alisema.

Meneja huyo alisisitiza Watanzania wanatakiwa kuendelea kumwombea kipa huyo kuhakikisha anapona kwa wakati na kurudi katika majukumu yake ya kawaida.

Camara alipata majeraha ya goti alipokuwa akiwania mpira langoni mwake katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), dhidi ya Gaborone United ya Botwana na kulazimika kutolewa nje.

Takwimu zinaonyesha Camara ameshacheza mechi 29 za CAFCL huku Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC), akifikisha mechi 16.

Katika hatua nyingine, Ahmed alisema kwamba wachezaji wengine wote waliokuwa katika majukumu ya timu zao za taifa, tayari walisharipoti kambini na kuanza mazoezi na wenzao tangu juzi.

Alisisitiza wapinzani wao Petro Atletico ya Angola, walitarajiwa kuwasili jana jijini Dar es Salaam kwa maandalizi ya mwisho ya mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL), utakaochezwa Jumapili katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

“Wachezaji wote waliokuwa katika timu zao za taifa tayari wamesharipoti kambini na kwamba wapinzani wetu Petro Atletico walitarajiwa kuingia nchini leo (jana) kwa ndege ya kukodi,” alisema Ahmed.

Katika michuano ya CAFCL, Simba imepangwa kundi D ikiwa na timu za Petro Atletico ya Anngola, Stade Milien ya Mali na Esperance ya nchini Tunisia.

Previous Post

YANGA ‘FULL’MZUKA CAFCL

Next Post

KOCHA SERENGETI BOYS AKOSHWA NA KIWANGO

Next Post
KOCHA SERENGETI BOYS AKOSHWA NA KIWANGO

KOCHA SERENGETI BOYS AKOSHWA NA KIWANGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WAZIRI MKUU ARIDHISHWA UJENZI BANDARI YA UVUVI KILWA

WAZIRI MKUU ARIDHISHWA UJENZI BANDARI YA UVUVI KILWA

4 months ago
USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

USHIRIKIANO WA CHINA NA AFRIKA KATIKA UJENZI WA RELI YA TAZARA

2 weeks ago

Popular News

  • MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    MUDATHIR KUIKOSA SIMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ‘MISS WORLD’ KUIPAISHA TANZANIA DUNIANI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • BIL. 195.66/- KUJENGA BONDE MTO MSIMBAZI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • ULEGA AJIBU MAPIGO KUHUSU MTANDAO WA BARABARA NCHINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • NEEMA YAJA, MIKAKATI HADHARANI KUINUA VIJANA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?