• ePaper
Thursday, April 16, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Burudani

YANGA, JS KABYLIE  NAMBA ZINAONGEA

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 26, 2025
in Burudani, Kimataifa, Michezo
0
YANGA, JS KABYLIE  NAMBA ZINAONGEA
0
SHARES
6
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na ABDUL DUNIA

WAKATI mechi za pili za hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) zikichezwa wiki hii, Yanga itakuwa na kibarua kizito kuhakikisha inavunja rekodi ya ushindi ya JS Kabylie katika dimba lake la nyumbani.

Yanga itachuana na JS Kabylie ya Algeria katika mechi ya kundi B itakayochezwa Ijumaa hii katika Uwanja wa Hocine Aït Ahmed, Tizi Ouzou nchini Algeria.

Katika mtanange huo wa aina yake, Yanga inayonolewa na Kocha Pedro Goncalves inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote kuendelea kukaa katika nafasi nzuri katika kundi hilo.

Hata hivyo, miamba hiyo kutoka mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo jijini Dar es Salaam, itakutana na kibarua kizito kuhakikisha inamaliza mechi bila ya kupoteza dhidi ya timu hiyo kutoka Algeria.

JS Kabylie katika dimba lake la nyumbani hadi sasa msimu huu, ina rekodi ya ushindi wa asilimia 100, ikishinda mechi mbili kati ya mbili ilizocheza katika hatua ya kwanza na ya pili za mtoano.

Katika hatua hizo za awali, JS Kabylie ilifunga jumla ya mabao saba na kuruhusu bao moja pekee katika uwanja wake wa nyumbani.

Ikiwa nyumbani, miamba hiyo ya Algeria ilipata ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Bibiani Gold Stars ya Ghana katika hatua ya kwanza na ushindi wa 2-1 ilipochuana na US Monastir ya Tunisia katika hatua ya pili.

Hata hivyo, Yanga nayo itaingia katika mtanange huo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao 3-0 ugenini iliyoupata dhidi ya Wiliete ya Angola katika hatua ya kwanza na kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Silver Strikers ya Malawi katika hatua ya pili ya mtoano.

Katika kundi B, Yanga ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi tatu sawa na kinara Al Ahly zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa, AS FAR Rabat ya Morocco inafuatia bila ya pointi sawa na JS Kabylie. Katika mtanange wa kwanza, Yanga ilishinda bao 1-0 dhidi ya AS FAR wakati JS Kabylie ikifungwa mabao 4-1 ilipocheza na Al Ahly.

Previous Post

YANGASC YAIFUATA KABYLIE KIBABE

Next Post

SIMBA YAPEWA MCHONGO

Next Post
SIMBA YAPEWA MCHONGO

SIMBA YAPEWA MCHONGO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

UN YAIFAGILIA TANZANIA KWA AMANI

UN YAIFAGILIA TANZANIA KWA AMANI

1 month ago
RAIS DK. SAMIA AWAKOSHA WABUNGE

RAIS DK. SAMIA AWAKOSHA WABUNGE

6 days ago

Popular News

  • PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    PROFESA IBRAHIM ATIA NENO TUME YA JAJI CHANDE

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SERIKALI YAFUTA LESENI 40 ZA UTAFITI  WA MADINI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TIMU OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WIZARA YA MAJI KUCHUANA MEI MOSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • SIMBA, FOUNTAIN GATE SIKU YA HESHIMA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • RAIS DK. MWINYI AKAGUA MJI WA AFCON FUMBA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?