• ePaper
Saturday, May 2, 2026
  • Login
No Result
View All Result
Uhuru Publication
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Hadithi
  • Login
No Result
View All Result
ePaper
Uhuru Publication
Home Habari

RAIS DK. SAMIA APONGEZWA UAMUZI SHEREHE ZA UHURU

Abdurahman Jumanne by Abdurahman Jumanne
November 27, 2025
in Habari, Kitaifa
0
RAIS DK. SAMIA APONGEZWA UAMUZI SHEREHE ZA UHURU

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan

0
SHARES
8
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

Na SIMON NYALOBI

BAADHI ya viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani nchini, wamepongeza uamuzi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kuelekeza fedha zilizotengwa kwa maadhimisho ya Sherehe za Uhuru za Desemba 9, 2025, zitumike kurekebisha miundombinu iliyoharibika kutokana na vurugu za Oktoba 29, mwaka huu.

Wakizungumza na Uhuru hili kwa nyakati tofauti, viongozi hao, walisema uamuzi huo, unapaswa kuungwa mkono kwa kuwa una tija kwa wananchi.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia Makini, Coaster Kibonde, alisema uamuzi huo ni busara na unapaswa kuungwa mkono na watu wenye mapenzi mema na nchi.

“Nampongeza Rais Dk. Samia kwa uamuzi sahihi, umelenga kumsaidia mwananchi wa kawaida ambaye kila siku, anaitumia miundombinu hiyo.

“Tukumbuke maadhimisho ya Sherehe za Uhuru yanapita, lakini miundombinu itatumika muda mrefu, ni mahitaji ya wananchi, tumpongeze Rais Samia kwa uamuzi huo,” alisema.

Alifafanua kwamba, kurekebishwa miundombinu ya mabasi ya mwendokasi, kutapunguza changamoto ya usafiri kwa wananchi wa kawaida, ambao hutumia kwenda katika shughuli za uzalishaji mali.

Katibu wa Chama cha Wakulima (AAFP), Rashid Rai, alisema uamuzi wake, umejali maslahi ya wananchi wengi.

“Uamuzi wake, umeonesha utumishi uliotukuka, fedha zinakwenda kutumika kutatua matatizo ya watu wengi, badala ya sherehe pekee,” alisema.

Alisema uamuzi wa Rais Samia, unathibitisha dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wengi waliompa ridhaa ya kuwaongoza katika kipindi cha miaka mitano.

Vilevile, aliyekuwa mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF) Jimbo la Ukonga, jijini Dar es Salaam, Rashid Mweyo, alisema uamuzi huo, ni sahihi kwa kuwa, fedha hizo zitagusa maisha ya wananchi wa kawaida.

Mwanasiasa huyo, alisema uamuzi huo utaponya ‘majeraha’ ya baadhi ya wananchi katika maeneo tofauti, wanaokosa huduma baada ya ofisi za serikali za mitaa na vituo vya polisi, kuchomwa katika vurugu hizo.

Previous Post

WAZIRI CHONGOLO AELEKEZA MIFUMO TOSCI ISOMANE

Next Post

KETE MUHIMU KWA YANGA LEO

Next Post
KETE MUHIMU KWA YANGA LEO

KETE MUHIMU KWA YANGA LEO

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Recommended

WADAU WANA MATARAJIO CHANYA NA TUME YA JAJI CHANDE

WADAU WANA MATARAJIO CHANYA NA TUME YA JAJI CHANDE

3 weeks ago
DK. NCHIMBI ATAJA FAIDA UKARABATI RELI TAZARA

DK. NCHIMBI ATAJA FAIDA UKARABATI RELI TAZARA

5 months ago

Popular News

  • TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    TANZANIA YAJINADI KIMATAIFA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • VYALENGA KUIJENGA JAMII KIUCHUMI NA KIROHO

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • KUVUMILIANA MUHIMU

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • WAZIRI SANGU ABAINISHA HIFADHI SKIMU INAVYOENDA KUBADILI MAISHA YA WATANZANIA

    0 shares
    Share 0 Tweet 0
  • TUCTA: WAAJILI WATEKELEZE NYONGEZA YA KIMA CHA MISHAHARA SEKTA BINAFSI

    0 shares
    Share 0 Tweet 0

Stay Update, Subscribe Now!

Check your inbox or spam folder to confirm your subscription.

Ukurasa Rasmi wa Televisheni ya Gazeti la Uhuru.

Facebook-f Instagram X-twitter Youtube tiktok
Quick Links
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalum
  • Kolamu
  • Makala
Services
  • ePaper
Contact Information
  • Dar es Salaam,Tanzania
  • info@upl.co.tz
  • +255 783 925 742
Uhuru Publications , 2025 © All Rights Reserved
  • Terms & Conditions
  • Privacy Policy
  • FAQ
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Michezo
  • Uchaguzi
  • Burudani
  • Toleo Maalumu
  • Kolamu
  • Makala
  • Contact
  • Hadithi

© 2026 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?